• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Wanafunzi Watoro kufuatiliwa

Posted on: September 1st, 2020

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Ndg, Frank Chonya amewaagiza watendaji wa vijiji vya Mkutingome na Namilema kuwafuatilia wanafunzi 28 wa darasa la saba ambao hawajaripoti katika kituo chao cha kambi Naunambe.

Ametoa tamko tarehe 31/08/2020 alipofanya ziara ya kutembelea kambi mbilii ya Naunambe na Mbekenyera zilizopo katika kata ya Mbekenyera.

Aidha, Mkurugenzi alimtaka Mkuu wa shule ya Naunambe kuacha kutoa ruhusa zisizo za lazima kwa wanafunzi hao wa darasa saba kwani kufanya hivyo kurudisha nyuma maendeleo ya wanafunzi hao,

“Tuna malengo yetu na ni lazima tuyafikie hatuwezi kuyafikia kama tutaendelea na utaratibu huu, tumekubaliana kufika asilimia 100 ya ufaulu kitaifa ili tufike hapo  wanafunzi kwa pamoja ni lazima wahudhurie darasani siku zote za kambi” amesema Chonya

Pia Mkurugenzi Chonya aliahidi kuwa kambi itakayofaulisha vizuri itazawadiwa shilingi laki mbili kama motisha yao na mwalimu mkuu wa shule ilipo kambi atapata motisha ya shilingi elf arobaini.

"Hizi ni ahadi ambazo nitatimizia mwenyewe bila shida yoyote, hivyo fundisheni wanafunzi wetu wafaulu mpate hizo fedha fanyeni mabadiliko walimu tusomeke kitaifa katika kumi bora” amesema Chonya.

Vile vile Ndg Chonya amewashauri walimu wakuu wa shule za Ruangwa kuchangia kiasi cha shilingi laki moja kutoka katika fedha zao za posho ya madaraka kwa ajili ya kuwanunulia chakula walimu wanaojitolea katika makambi.

“Halmashauri imetoa chakula kwa ajili ya walimu hao si vibaya na wakuu wa shule wakaonyesha uzalendo, mwalimu anapaswa asiwaze wala asiwe na shida ya chakula ili ufundishaji wake uzidi kuimarika” amesema Chonya.


Naye Mratibu elimu kata Jofrey Robert Manase ameushukuru uongozi wa kijiji cha Mbekenyera kwa kuwapa ushirikiano katika kambi ya Mbekenyera kwa kuwavutia umeme katika madarasa wanayosomea wanafunzi hao.

Mratibu huyo kwa niaba ya walimu waliopo katika kambi ya Naunambe na Mbekenyera alimuhakikishia Mkurugenzi Kuwa watafanya vizuri na kufikia malengo ya asilimia mia ufaulu kitaifa.

Wilaya ya Ruangwa ina jumla ya kambi 21 ambazo zipo katika shule zote zilizopo ndani ya Ruangwa.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA YAPATA USAJILI KWA MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA (CPD)

    November 20, 2025
  • MHE NGOMA AWAPONGEZA NMB KWA KUIPANDISHA THAMANI YA KOROSHO KWA WANANCHI WA RUANGWA

    November 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA LISHE KITAIFA 2025

    November 15, 2025
  • MAAFISA UTAMADUNI WAKUTANA NA WALAMBO, NGARIBA NA WAMILIKI WA VIWANJA VYA JANDO NA UNYAGO

    November 14, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa