• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Vijana Wilayani Ruangwa Wapongezwa na Wajumbe wa ALAT

Posted on: April 17th, 2018
Wajumbe na viongozi wa jumuiya ya serikali za mitaa Tanzania (ALAT)  Mkoa wa Lindi, wamefika WIlayani Ruangwa Mkoani humo kwa lengo la kufanya mkutano wa kujadili maendeleo ya mkoa huo na kutembelea miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi unaondelea wa uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa WIlayani Ruangwa.


Akizungumza wakati walipotembelea ujenzi wa uwanja huo na kuona vijana walioamua kufyatua tofali kwa kujitolea uwanjani hapo, Mwenyekiti wa ALAT Mkoani Lindi ambae pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya WIlaya Ruangwa mh. Rashid Nakumbya amewashukuru vijana hao kwa kujitoa katika shughuli za kimaendeleo na kusisitiza kuwa kwa sasa wana Ruangwa na Lindi kwa jumla tunazungumza lugha moja ya maendeleo na si vinginevyo.


Nakumbya ameleeza kuwa Mkoa wa lindi ni miongoni mwa Mkoa ambayo inatajwa kuwa nyuma kimaendeleo na hivyo kueleza kuwa katika vikao vyao (ALAT) Mkoa  wamekua wakihakikisha wanapambana na kuweka mikakati ya kuhakikisha mkoa huo unatoka nyuma na kusogea mbele.


“ na katika kusogea mbele hakuna ubaguzi ndio maana wako hapa leo na wote wanaunga mkono maendeleo, na ni imani yangu vijana watatumika zaidi kuhamasisha maendeleo katka maeneo yao” alisema, nakumbya wakati akizungumza na vijana pamja na wajumbe waliofika kutembelea uwanja huo.


Naye Katibu wa vijana walijitolea kufyatua tofali kwa ajili ya ujezi wa ukuta wa uwanja huo bw.Ibrahim Joshua, amesema wameamua  kuhamasisha vijana kutoka vijiji vyote wilayani humo na kukubali kujitolea kufika uwanjani hapo kuendesha shughuli ya awali ya ufyatuaji tofali kwa ajili ya ujenzi wa ukuta wa uwanja huo wa kisasa unaotegemewa kukamilika mwishoni mwa mwezi wa saba.


Amesema awali kambi yao ilipangwa kumalizika kwa muda wa siku saba lakini kutokana na umuhimu wake kuonekana bado vijana walikua na hari wakaongeza siku mbili ili kukamilisha ili kumalizia idadi ya mifuko ya sementi  iliyokuwapo uwanjani hapo.


“vijana wapo tayari kutumikia jambo hili siku yeyote, na ndiyo maana leo ndio siku ya mwisho ya awamu ya kwanza ya kujitoa kwa ajili ya ujenzi huu kwa maana ya kwamba kufyatua tofali, lakini jumapili tunarud tena kwahiyo ni ishara kwamba vijana hawa wamejitoa kwa moyo wao thabiti” amesema ibrahim.


Aidha kwa upande wa wajumbe wa (ALAT) Lindi walifika kutembelea mradi huo wa ujenzi wa uwanja, wamefurahishwa kwa kuona vijana hao wamejitoa kwa ajili ya kufanikisha ufyatuaji wa tofali kwa ajili ya  ujenzi wa uwanja huo bila malipo, huku wakieleza kuwa jambo hilo linasogeza kasi ya maendeleo na kusema kuwa ni jambo la kujifunza na kuiga kwa kujivunia.


Jumla ya mifuko ya sementi 422(mia nne ishirini na mbili) iliozalisha tofali 7871 (elfu saba mia nane sabini na moja) imefyatuliwa na vijana hao ambao wameweka kambi uwanjani hapo kwa muda wa siku tisa ili kusaidia kuongeza kasi ya kufanikisha kukamilika kwa ujenzi wa kuta za uwanja huo. Uwanja huo unaendelea kujengwa wilayani ruangwa ambao umepewa jina la majaliwa vibrant play ground unategemewa kukamilika mwishoni mwa mwezi wa saba mwaka huu ili mwanzoni mwa mwez wa nane uanze kutumika kwa kutimua kivumb katika mashindano la ligi daraja la kwanza Nchini.

Mwisho


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa