• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

VETA YATOA MAFUNZO YA UFUGAJI KUKU NA SAMAKI KWA WAJASILIAMALI WILAYANI RUANGWA.

Posted on: May 23rd, 2022

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mw. George Mbesigwa amewataka washiriki wa mafunzo ya ufugaji kuku na samaki kwenda kutekeleza mafunzo hayo kwa vitendo na pia kuwarithisha wananchi wengine ujuzi mliopata.  

Aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku tano  yaliyofanyika katika chuo cha VETA cha wilaya ya Ruangwa ambapo jumla ya washiriki 264 kutoka kata 9  walinufaika na mafunzo hayo. Kata hizo ni  Nandagala, Malolo, Likunja, Ruangwa, Nachingwea, Namahema, Chienjere, Nkowe na Mnacho

VETA imekuwa ikitoa mafunzo hayo kupitia mfumo uitwao (INTEP Integrated Training for Entrepreneurship Promotion) ikiwa lengo ni kuandaa na kujengea uwezo wajasiliamali wadogo ili waweze kukua na kuongeza ufanisi na tija katika biashara zao na hatimae kuongeza kipato katika ngazi ya familia, jamii na taifa kwa ujumla.

"Mafunzo haya yangeweza kupelekwa sehemu nyingine ila yameletwa Ruangwa hivyo ni wajibu wenu kuyafanya mafunzo haya kuwa endelevu, nendeni mkafuge kuku na samaki kama ulivyofunzwa" amesema Mbesigwa

Pia aliwataka washiriki kuendeleza elimu na ujuzi waliopata katika mafunzo na kwa sababu mshiriki anaweza kufuga kuku na samaki na akaendelea kufanya shughuli nyingine za kujiongezea  kipato lakini pia kukidhi kiu ya uhitaji ya wana Ruangwa.

Aidha aliuomba uongozi wa VETA Kanda ya Kusini Mashariki kuhakikisha kuwa Kata 13 zilizobaki zinapatiwa mafunzo kama haya au mengineyo ili kuisaidia jamii yote kujikomboa kiuchumi.

Kuhusu mafunzo katika chuo cha VETA cha wilaya ya Ruangwa alisema;  vijana na wazazi wenye wenye vijana wenye sifa na waliochaguliwa kujiunga wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo ya kufika chuo mapema maana ikitokea mtu hajafika basi nafasi yake atapewa mtu mwingine.


"Tumejulishwa kuwa  Chuo cha VETA cha Wilaya ya Ruangwa kitaanza kutoa mafunzo  mwezi wa 6. Hivyo  vijana waliochaguliwa  mjiandae mapema msijepoteza nafasi hii kwani msipokuja nafasi hii watapewa vijana wa  maeneo mengine" amesema Mbesigwa.

Naye mratibu wa Mafunzo Prosper Sacky (mtafiti wa soko la ajira) Kutoka ofisi ya VETA Kanda alielezea amevutiwa sana na mwitikio wa washiriki katika wilaya Ruangwa tofauti na  sehemu nyingine mabazo aina hii ya mafunzo yamefanyika. ambapo kwa kawaida hunaojitokeza ni kati ya 20 hadi 30. lakini  kwa wilaya Ruangwa walioomba kupata mafunzo walikuwa ni takribani 637 na walionufaika katika awamu hii ni 264.

Aliendelea kusema kutokana na mwitikio huu wa wananchi kuona thamani ya kupata elimu ili kujijengea uwezo,  unemfanya atamani kurudi tena Ruangwa kwa ajili ya mafunzo mengine kadri ya uhitaji.

 Pia alisisitiza umuhimu wa kujiandaa kutumia fursa zitakazotokana na ujenzi wa barabara ya Ruangwa hadi Nanganga na pia  matarajio ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata gesi asilia kinachotarajia kujengwa Lindi kwani kutakuwa na ongezeko la mahitaji hususani vyakula,


Naye Kaimu Mkurugenzi wa VETA kanda ya kusini Bwana Elias Nzunda aliwapongeza wana Ruangwa kwa kuitikia mwito wa kupata mafunzo ili kujiongezea kipato. Aliwasisitiza kutumia chuo cha VETA cha wilaya Ruangwa ili kujikwamua kiuchumi na kwamba chuo cha VETA Ruangwa kitumike vyema kwani fani zilizopangwa kuanza zitawajenga vijana katika kuikwamua wilaya ya Ruangwa. 

Pia alishukuru serikali ya Jamhuri wa Muungani wa Tanzania kupitia uongozi wa rais Samia Hasani Suluhu katika kujenga Tanzania ya wajasiliamali wenye ujuzi. Pia alimshukuru Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na (Mbunge wa Ruangwa) Mh. Kasim Majaliwa (Mb) kwa kusimamia vyema na kwadhati miundominu na maendeleo ya wana Ruangwa. Aliwasihi washiriki wa mafunzo kwenda kuwa mabalozi katika kukitangaza chuo cha VETA Ruangwa ili vijana wengi wajitokeze kujiunga na hatimae waendeleze uchumi wa wana Ruangwa.

Nao washiriki wa mafunzo walitoa risala yao ambayo wakimshukuru Rais samia Suluhu Hasa raisi wa  serikali ya Muungani wa Tanzania na pia mbunge wao na waziri mkuu Mh. Kasim Majaliwa kwa kuwakumbuka na kuahidi kwambamafunzo waliyopata watayafanya kwa vitendo. Pia waliomba oungozi wa VETA ue karibu nao na kuendelea kuwalea ili hatimae  waweze kufikia ndoto na malengo yao.  

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa