• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Utoro haukubaliki tunaenda kuchukua hatua

Posted on: February 5th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Ruangwa Mhe. Hassan Ngoma ameagiza viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha watoto ambao hawajaripoti shule wanafanya ivyo na kuanzia tarehe 14/02/2022  mtoto ambaye hajafika shule hatua za kisheria zichukuliwe kwa yeyote anayehusika ikiwemo mtoto mwenyewe.

Amesema hayo wakati wa baraza la madiwani la kawaida la robo ya pili lililofanyika tarehe 05/02/2022 katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya Ruangwa mjini.

Amesema wiki ijayo atafanya msako kijiji kwa kijiji nikiwa ameambatana na mgambo ambao watakamata watoto hao watoro.

"Kama kuna mzazi anasababisha mtoto wake asifike shule kwa makusudi, acha mara moja elimu ni haki ya mtoto wako na nikibaini wapo wazazi wa hivyo tutawafikisha mahakamani" amesema Ngoma

Aliendelea kusisitiza Mkuu wa wilaya kuwa suala la uachaji shule na utoro holela umekithiri Ruangwa nitahakikisha nakomesha hili suala.

"Waheshimiwa madiwani nendeni mkatusaidie kuongea na wananchi katika maeneo yenu, watoto ambao hawajafika shule wafike shule mara moja tukimkatama mtoto ambaye hajafika shule huyo tunamfikisha mahakamani siku hiyo hiyo" amesema Ngoma

Naye Diwani wa kata ya Mandawa Mheshimiwa Lipei kwa niaba ya madiwani wote alisema suala la shule ni lazima na si hiyari na hata kama hao watoto wamewazaa wao ni lazima wawasomeshe.

"Sisi tunatekeleza ilani na mkuu wa Wilaya tutakupa ushirikiano katika kutafuta hawa watoto watoro hatuwezi kufumbia macho mambo muhimu kama hayo ya elimu" amesema Lipei.

Alisema Mheshimiwa Lipei sisi ni viongozi ila ni wazazi pia, kumuona mtoto anaacha shule kwa makusudi haivumiliki hivyo tutakusaidia kuhakikisha wanarudi shule.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa