• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

UJENZI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM TAWI LA RUANGWA KUKAMILIKA NDANI YA MIEZI 18

Posted on: July 9th, 2024

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam ambaye ni Mratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa mageuzi ya Uchumi Profesa Bernadeta Killiani amesema kwamba Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam tawi la Ruangwa watahakikisha ndani ya miezi 18 Mkandarasi anakabidhi majengo.


Ameyasema hayo leo Julai 9, 2024 katika Kikao kazi cha uzinduzi wa Kamati ya "Kasema" itakayoshirikiana na Mradi wa Elimu ya Juu kwa mageuzi ya Uchumi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri.


Aidha, Profesa Killiani ametoa wito kwa wananchi wa Ruangwa kuonesha ushirikiano kwani mafanikio ya Mradi yanategemea muamko na ushirikiano na wanachi wa eneo husika.


Kamati ya "Kasema" ina Wajumbe watano na ina lengo la kukusanya na kushughulikia maoni au malalamiko ya wananchi katika eneo husika kuhusu Mradi.


Pia, ina lengo la kuweka kumbukumbu za kile kinachofanyika katika Mradi, na ni sehemu ya Ulinzi na Usalama wa Mradi huo.


Mradi wa Elimu ya Juu kwa mageuzi ya Uchumi chini ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam umefadhiliwa na Mkopo wa Benki ya Dunia na utekelezaji wake ni katika maeneo mapya 14, na mpaka sasa maeneo mapya matatu tayari yameshafikiwa ambayo ni Ngongo (Lindi Manispaa), Likunja (Wilaya ya Ruangwa) pamoja na Kagera.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Andrew Chikongwe ameushukuru Uongozi wa Kata ya Likunja kwa kutoa Hekari 400 ambapo Kitivo cha Kilimo kitajengwa.


Aidha, Mhe Chikongwe ameendelea kwa kusema kuwa Mradi huu ni chachu ya maendeleo wilayani Ruangwa kwa sababu wananchi watajifunza namna ya kuongeza uzalishaji, idadi ya watu pia itaongezeka na hii itaenda kubadili sura ya Wilaya ya Ruangwa.


Pia, ametoa wito kwa wakazi wa Kata ya Likunja wajenge nyumba bora na za kisasa, kulima vizuri na kisasa zaidi ili kuongeza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Halmashauri kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa