• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Uadilifu unahitajika ili misitu iwe endelevu na mapato yawe ya uhakika

Posted on: July 12th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mheshimiwa Hassan Ngoma ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uvunaji Wilaya, Amewataka wavunaji wa misitu kuwa waadilifu na kuvuna kiasi kinachoridhiwa na kamati ya uvunaji wa misitu.

Amesema "kumekuwa na tabia ya wavunaji kuomba idadi kubwa ya miti kisha kuvuna michache, hali hii inasababisha hoja za ukaguzi katika mapato kwani vijiji hukadiriwa makusanyo makubwa kutokana na uvunaji. kutovuna miti kwa idadi wanazoomba inaleta tofauti kubwa katika mapato halisi na yaliyotarajiwa.

Amesema hayo wakati wa kikao cha Kamati ya Uvunaji Wilaya kilichofanyika tarehe 12/08/2022 ikiwa ni kikao cha kwanza cha mwaka wa fedha 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya Ruangwa mjini.

Amewataka wavunaji wa misitu kufuata sheria na taratibu za uvunaji ili kutunza misitu hiyo na kuhakikisha inakuwa endelevu. Mhe. Mkuu wa Wilaya  amekemea na kusisitiza wafanyabiashara wote kuacha kusafirisha mbao na magogo wakati wa usiku.

Aidha Mhe. Mkuu wa wilaya ametoa agizo kwa vijiji vyenye migogoro ya ardhi kuhakikisha migogoro hiyo inasuluhishwa kwa kukutana na kufanya mazungumzo ambayo yatapelekea makubaliano ya kuimaliza.

Akianisha migogoro hiyo  Mhe. Mkuu wa Wilaya ametaja kijiji cha Namiegu na Nandeje, Mtondo na Nanjaru, Lichwachwa na Nahanga. Ameagiza kupewa taarifa ya hatua waliyofikia katika kutatua migogoro hiyo kabla ya tarehe 1/08/2022

"Naagiza wenye migogoro wakutane, wajadiliane na wasuluhishe kabla ya tarehe hiyo maana ikifika tarehe hiyo na bado mnaendeleza kuzozana nitatuma timu ya wataalamu waje wawaonyeshe mipaka ilipo kwa kufuata taratibu na sheria. Nafasi ya kupata suluhu kwa majadiliano mnayo, naomba muitumie"

Aidha alishukuru vijiji vilivyotoa  mbao kwa ajili ya kujenga mabanda ya wafanyabiashara wadogo. Mabanda hayo yameboresha mazingira ya biashara kwa watu wetu pamoja na kuongezeka kwa makusanyo ya Halmashauri.

"Mmeonesha uzalendo na kuipenda Ruangwa yetu, mmerahisisha zoezi la upatikanaji mbao na mmerahisisha zoezi la ujenzi wa vibanda hivyo ambavyo vinatumika na wafanyabiashara wadogowadogo" amesema Ngoma.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa