• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

TFCG na MJUMITA wafikisha elimu ya usimamizi wa fedha kwa wavunaji mbao na wachoma mkaa

Posted on: July 2nd, 2022

Afisa anayesimamia Mradi wa  uzalishaji mkaa kwa kutumia Teknolojia iliyoboreshwa Ndg. Othman Lugendo   ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo ya uchomaji mkaa na upasuaji mbao kufuata taratibu zilizowekwa ikiwemo kukata leseni za biashara ili  kurasimisha shughuli zao.

Amesema, sasa ni wakati muafaka wa wafanyabiashara hao kutumia walichofundishwa na kuhakikisha shughuli zao zinatunza mazingira wakati  zikiwasaidia kujikwamua kiuchumi.

Amesema hayo leo tarehe 02/07/2022 wakati wa mafunzo ya usimamizi wa fedha kwa wavunaji mkaa na mbao kwa kutumia teknolojia iliyoboreshwa yaliyofanyika ofisi ya kijiji cha Malolo.

"elimu mliyopata inapaswa kuanza kufanya kazi, natamani kuona nilichofundisha kipindi chote cha mafunzo haya kinawasaidia, natamani nikirudi nione mabadiliko ya mtu mmoja mmoja na kijiji kwa ujumla"

Faida zingine zinazotarajiwa kutokana na mradi ni kuongezeka kwa mapato ya kijiji ambayo itasaidia  kukamilisha na kuanzisha miradi mbalimbali katika kijiji hicho.

Akihitimisha nasaha zake alisisitiza baada ya kukata leseni na kuwa kikundi rasmi wanaweza kuanza kuomba mikopo ya  wanawake na Vijana inayotolewa na  Halmashauri ili iweze kuwasaidia kuendeleza kazi zao.

Naye kaimu Afisa ardhi na maliasili ndugu Isihaka Panja aliushukuru uongozi wa Shirika la kuhifadhi misitu asili Tanzania (TFCG)  na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania ( MJUMITA) kwa kuwapelekea mafunzo hayo wananchi wa Malolo kama kijiji cha mfano.

Amesema Ndg Panja kazi wanazofanya washiriki hao zinahitaji sana mshikamano hivyo washikamane ili waweze kufanya kazi kwa uharaka na urahisi.

Aidha amesema wanachama wa vikundi hivyo wanapaswa kuanza kufanya kazi sasa kwani mabadiliko yanaanza sasa na si baadae.

"mnapaswa kuanza uchomaji na uvunaji mbao kwa kufuata taratibu mlizoelekezwa".

Mafunzo hayo ni muendelezo wa mafunzo waliopata washiriki kwa vitendo yanayoratibiwa na Shirika la Kuhifadhi Misitu Asili Tanzania (TFCG) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA)


MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa