• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

TARI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA KILIMO CHA MINAZI RUANGWA

Posted on: April 15th, 2025




Kituo cha Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kupitia tawi lake la Mikocheni, kimeonesha kuridhishwa na maendeleo ya kilimo cha minazi wilayani Ruangwa, mkoani Lindi, baada ya kufanya ziara leo Aprili 15, 2025. ya kukagua mashamba ya minazi iliyoanzishwa kwa ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya hiyo.


Ziara hiyo ni sehemu ya ufuatiliaji wa kitaalamu wa utekelezaji wa mpango wa kuendeleza zao la mnazi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, ambapo miche ya minazi ilisambazwa kwa wakulima ili kuinua kipato chao na kuimarisha uchumi wa maeneo ya pwani kwa ujumla.


Naye, Mratibu wa Uhaulishaji wa Teknolojia na Mahusiano kutoka TARI Mikocheni, Bi. Vidah Yosia Mahava, ambaye ameongoza ziara hiyo, amesema kuwa wakulima wameonesha juhudi kubwa katika kutunza miche hiyo na wameitikia vyema teknolojia waliyopewa. 


“Tunaona maendeleo mazuri sana ya minazi hii, wakulima wameonesha moyo wa kujituma na wameitikia vyema teknolojia na elimu waliyopewa. Hili ni jambo la kufurahisha na linatupa matumaini makubwa kuhusu mustakabali wa zao hili,” amesema Bi. Mahava.


Katika ziara hiyo, wataalamu wa TARI wametembelea mashamba ya wakulima na kushuhudia hali ya miche, huku wakitoa pongezi kwa juhudi zinazofanywa na wananchi katika kuitunza. Wamewasihi wakulima kuendelea kufuata mbinu bora za kilimo ili kuhakikisha miche hiyo inakua kwa mafanikio na kuleta matokeo chanya.


Aidha, Bi. Mahava amesisitiza kuwa TARI itaendelea kutoa msaada wa kitaalamu na kufuatilia maendeleo ya minazi hiyo ili kuhakikisha mpango huo unaleta tija kwa wakulima. 


Ikumbukwe, Zao la mnazi linaelezwa kuwa na faida mbalimbali zikiwemo uzalishaji wa nazi, mafuta, mbao na bidhaa nyingine, hivyo kuwekeza katika zao hilo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuendeleza kilimo chenye tija.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa