• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Somesheni watoto wakike kwa manufaa ya taifa- Mhe Nakumbya

Posted on: March 8th, 2019

Katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Rashidi Nakumbya, ambaye alikuwa ni mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, amewataka wazazi kuelekeza zaidi nguvu kwa watoto wa kike kwa kuwapa elimu bora na kuwatengenezea mazingira salama ya kuishi.

Amesema hayo leo 08/03/2019  wakati wa maadhimisho ya Siku ya wanawake yaliyofanyika mjini Ruangwa katika kiwanja cha CWT.

Mheshimiwa Nakumbya amesema kumuendeleza kielimu mtoto wa kike kuna faida maana mtoto wakike anaweza kusoma mpaka elimu ya juu na bado akakumbuka kuisaidia familia yake.

Pia ametoa rai kwa wanaume kuwaruhusu wake zao kujishughulisha na shughuli za kimaendeleo kwa manufaa ya familia nzima ,wanaume tunajichelewesha kuwakataza wanawake wasifanye kazi au shughuli yoyote ya kuingiza kipato tunasahau kuwa maisha ni kusaidiana,  mwanamke anapopata  basi familia nzima inakuwa imepata.

Pia amewataka wanawake kutumia fursa wanazozipata kwa ufasaha na kuacha kufanya matumizi ya fedha bila mpangilo, vikoba vinawasaidia wanawake ila kuna wengine mmeanza  vitumia vibaya  mnakopa kurudisha inakuwa shida hembu fuateni taratibu za kukopa, kutumia na kurudisha kama mnavyoelekezwa

Vile vile amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi kwani kiongozi mwanamke mara nyingi huwa ni muadilifu

Naye Diwani wa viti maalumu Paulina ametoa rai kwa wanaume kuwaachia wanawake uhuru wa kujishugulisha katika kutafuta kipato ili kusaidiana majukumu ya ndani.

Naye mwanamke aliyepata zawadi ya kuwa mwanamke shupavu kwa ujasiriamali Anusyata Cosmas ameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa mikopo na elimu wanayowapatia wajasiriamali katika kikundi chao.

Bi Anusyat amewataka wanawake kutokata tamaa kwani ujasiriamali unalipa kama zilivyo kazi nyingine na kupitia ujasiriamali huo ameweza kujenga nyumba na kusomesha mtoto wake shule ya binafsi.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA YAPATA USAJILI KWA MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA (CPD)

    November 20, 2025
  • MHE NGOMA AWAPONGEZA NMB KWA KUIPANDISHA THAMANI YA KOROSHO KWA WANANCHI WA RUANGWA

    November 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA LISHE KITAIFA 2025

    November 15, 2025
  • MAAFISA UTAMADUNI WAKUTANA NA WALAMBO, NGARIBA NA WAMILIKI WA VIWANJA VYA JANDO NA UNYAGO

    November 14, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa