• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Serikali Yatoa Bilioni 1.4 Kuboresha Vituo vya Afya

Posted on: March 5th, 2018

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa, Serikali imetoa tsh.billioni 1.4 kwa ajili ya uboreshaji wa vituo vya afya katika wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.

Ameyasema hayo wakati alipotembelea kata ya mandawa kwa ajili ya kukagua mradi wa uboreshaji wa kituo cha afya cha kata hiyo wakati wa Ziara yake ya kikazi Wilayani humo.

“Serikali imeamua kuimarisha sekta ya afya kwa kujenga na kuboresha vituo vya afya li kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na kwa karibu na makazi yao.” Amesema Waziri Mkuu

Mhe. Waziri Mkuu amesema kati ya fedha hizo sh. Million 400 kwa ajili ya kituo cha afya Mandawa, sh. Milioni 500 kituo cha afya Mbekenyera na sh. Milioni 500 kituo cha afya Nkowe.

Amesema uboreshaji huo unahusisha ujenzi huo chumba cha upasuaji, maabara, chumba cha kujifungulia kina mama, wodi ya mama na mtoto na wodi ya wanawake na wanaume na chumba cha kuhifadhia maiti.

Aidha, Mhe. Majaliwa amewataka wananchi hao waendelee kuiunga mkono serikali yao, ambayo imedhamiria kuwatumikiaili waweze kupata maendeleo.

Pia Waziri Mkuu amekabidhi gari la kutolea huduma za afya vijijini. Gari hilo linauwezo wakutoa huduma za afya kama Zahanati kwani lina vitanda vitatu vya kulaza wagonjwa na litakuwa linatembea na manesi na daktari kwa ajili ya kutoa huduma.

“Huduma ya afya inazidi kuimarika kuanzia sasa kutakuwa na gari linaloenda katika vijiji vilivyombali na zahanati kwa ajili ya kuwapatia wananchi huduma umsiliogope kwani ni kama zahanati zetu” amesema Waziri Mkuu.

Katika hatua nyingine, Mhe. Waziri Mkuu ameshiriki katika zoezi la ufyatuaji wa matofali kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Kata ya Matambalale ambayo itakuwa inahudumia Vijiji visivyopungua vinne.

Amesema kata hiyo yenye vijiji vinne ilikuwa haina shule ya sekondari,hivyo kusababisha wanafunzi kutembea umbali wa kilomita tano kwenda kusoma kwenye shule za kata nyingine.

“Serikali inataka kumlinda mtoto wa kike apate elimu bila usumbufu wowote awali watoto wa kike wa kata ya matambalale walikuwa wanatembea umbali mrefu au kupanga mitaani hali ambayo inahatarisha usalama wao, baada ya kukamilika ujenzi wa shule hii watoto wakike watasoma katika mazingira mazuri” amesema Waziri Mkuu

Naye mwanakijiji wa kata wa Matambarale bi Zuhura Idi amesema wanaushukuru uongozi wa Halmashauri kwa kuona jinsi watoto wao wanavyopata shida na kuamua kuwasaidia katika kuhakikisha inapatikana shule ya sekondari katika kata hiyo.

“Wananchi wa kata ya Matambarale tutashirikiana na uongozi wa halmashauri kwa hali na mali katika kufanikisha zoezi hili la ujenzi wa shule kukamilika kwani watoto wetu hasa wa kike wanapata elimu katika mazingira magumu”amesema bi Zuhura.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa