• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Ruangwa yatoa mikopo ya vifaa vya sh.milioni 357 kwa wajasiriamali

Posted on: February 27th, 2021


Waziri Mkuu   Kassim Majaliwa amekabidhi vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 357 kwa vikundi vitano vya wajasiriamali vilivyotolewa kwa mkopo na Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa ikiwa ni asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. 

Pia, Waziri Mkuu amepokea msaada wa madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka katika Kampuni ya vinywaji baridi ya Cocacola Kwanza ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Waziri Mkuu amekabidhi vifaa hivyo leo Februari 27, 2021 katika viwanja vya shule ya msingi Likangara wilayani Ruangwa na kuwataka wanufaika wa mikopo hiyo wakaitumie kama ilivyokusudiwa na wahakikishe wanarejesha kwa wakati.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kuamua kutoa mikopo ya vifaa mbalimbali kwa wajasiriamali na pia ameitaka ihakikishe inawasimamia vizuri wanufaika hao.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Frank Chonya amesema halmashauri yao imeendelea kutenga na kutoa mikopo kwa vikundi vya ujasiriamali vya wanawake, vijana na wenye ulemavu kupitia asilimia 10 ya makusanyo ya mapato ya ndani.

Mkurugenzi huyo amesema kwa mwaka 2020/2021 halmashauri ya wilaya ya Ruangwa imetoa mikopo mikubwa yenye thamani ya shilingi milioni 357 ambazo wanavikundi wamenunua vifaa kwa ajili ya shughuli zao na wengine wameanzisha biashara ndogondogo.

Amesema halmashauri ilifanya utafiti na kuunda vikundi vitano vya kimkakati ambavyo vimepewa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 319,910,000. ”Vikundi viwili vyenye wanufaika 20 ambavyo vinavyojishughulisha na ufugaji wa kuku vimepewa mkopo wa shilingi 13,010,000 na wamenunua kuku 2,000 aina ya chotara.”

”Kikundi kingine ni cha vijana 39 wanaofyatua matofali ambacho tumekipa mkopo wa shilingi milioni 186, ambapo wameweza kununua lori la tani nane la kusombea mchanga na kubebea tofali, mtambo wa kufyatulia tofali, mifuko ya saruji 600 na fedha zingine ni kwa ajili ya shughuli za uendeshaji.”

Amesema kuwa kikundi kingine kilichonufaika na mkopo huo ni Jukwaa la Wanawake Ruangwa lenye wanufaika 37 ambalo linajishughulisha na usafi wa mazingira lililopewa mkopo wa shilingi milioni 72.5 ambazo wamezitumia kwa kununua trekta na tela lake na vifaa vya kufanyia usafi. Kikundi hicho kinafanya usafi kwenye mji wa Ruangwa.


 Mkurugenzi huyo amesema kikundi kingine kilichonufaika na mkopo huo ni cha vijana 10 wanaojishughulisha na uendeshaji wa bodaboda na bajaji ambao wamepewa mkopo wa shilingi milioni 48.4 na wameweza kununua bajaji tano na pikipiki nne.

Baada ya kupokea vifaa hivyo wanufaika hao waliishukuru Serikali kupitia ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa kwa kuamua kuwakopesha vifaa kwa kuwa vitawezesha kuboresha shughuli zao za ujasiriamali na kwamba watahakikisha wanarejesha fedha hizo kwa wakati ili wananchi wengine waweze kunufaika.

MWISHO

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa