• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

RUANGWA YAPOKEA KUKU 1,000 KUTOKA TALIRI KWA AJILI YA MRADI WA UFUGAJI SHULE YA MSINGI NANDAGALA

Posted on: July 5th, 2025

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nandagala wilayani Ruangwa wanatarajiwa kuanza kupata lishe bora kupitia mpango wa lishe shuleni baada ya kukabidhiwa kuku 1,000 aina ya Hyline Brown, kupitia Mradi wa School Feeding Eggs Program unaotekelezwa na Kituo cha Utafiti wa Mifugo Tanzania Kanda ya Kusini (TARLI), kwa ufadhili wa Ofisi ya Sapling IRLI.


Akizungumza leo Julai 5, 2025 kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TARLI, Mkurugenzi wa Utafiti Dkt. Andrew Chota, amesema kuwa mradi huo unalenga kuimarisha afya za watoto kwa kuwapatia protini ya kutosha, kuwajengea stadi za maisha, pamoja na kuongeza kipato kwa shule.


“Kuanzia wiki ya 24 ya kuku hawa, kila mwanafunzi katika Shule ya Msingi Nandagala ataanza kupata yai moja kwa siku. Hii ni hatua kubwa katika kuhakikisha watoto wanakuwa na afya bora na uwezo mzuri wa kujifunza,” amesema Dkt. Chota.

Aidha, Dkt. Chota ameeleza kuwa wataalamu wa TARLI wataendelea kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa mradi huo kwa kuhakikisha usafi wa banda, utoaji wa chanjo kwa wakati na maendeleo ya afya ya kuku hao ili kuwaepusha na magonjwa.


Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndg. Zuberi Sarahani, mara baada ya kupokea rasmi kuku hao kwa niaba ya Halmashauri, ametoa shukrani zake za dhati kwa wafadhili hao, akisisitiza kuwa Serikali ya Kata pamoja na Uongozi wa Shule wanapaswa kusimamia mradi huo kwa makini ili kuleta tija iliyokusudiwa.


“Mradi huu si tu wa kutoa mayai, bali unajenga kizazi cha vijana wenye afya bora, wanaojifunza kwa vitendo stadi za maisha, na kuisaidia shule kujitegemea,” alisema Ndugu Sarahani.


Wazazi, walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Nandagala wamepokea mradi huo kwa shangwe na matumaini makubwa, wakisema kuwa utasaidia kupunguza utapiamlo kwa watoto na kuongeza ari ya mahudhurio darasani.


Mradi wa School Feeding Eggs Program ni mfano wa ubunifu unaoonyesha namna tafiti za kisayansi na ushirikiano wa taasisi za Serikali na binafsi zinavyoweza kutatua changamoto za msingi katika elimu na afya za watoto mashuleni.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • RUANGWA YAPOKEA KUKU 1,000 KUTOKA TALIRI KWA AJILI YA MRADI WA UFUGAJI SHULE YA MSINGI NANDAGALA

    July 05, 2025
  • TASAF KUTOA RUZUKU KWA KAYA 3,896 RUANGWA KUANZIA JULAI 2

    July 02, 2025
  • RUANGWA YAPOKEA DOZI 12,500 ZA CHANJO ZA MIFUGO

    June 27, 2025
  • WILAYA YA RUANGWA KUNUFAIKA NA MRADI WA URASIMISHAJI MAKAZI HOLELA

    June 24, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa