• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

RUANGWA YAFANYA KONGAMANO MAALUM MAADHIMOSHO YA MIAKA 63 YA UHURU

Posted on: December 6th, 2024


Wilaya ya Ruangwa leo tarehe 6 Desemba 2024, imefanya kongamano maalum kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara, likihudhuriwa na makundi mbalimbali kutoka sekta ya umma na binafsi, wanafunzi, viongozi wa dini, kamati ya siasa ya Wilaya, na wawakilishi wa kundi la wenye ulemavu.


Mgeni rasmi wa kongamano hilo alikuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Mheshimiwa Andrew Chikongwe, ambaye ametumia fursa hiyo kupongeza mafanikio makubwa ya kiuchumi yaliyopatikana tangu uhuru. “Tumepiga hatua kubwa sana tangu uhuru mpaka leo,” amesema Chikongwe, akiweka msisitizo kwenye maendeleo yaliyoshuhudiwa ndani ya Wilaya ya Ruangwa na taifa kwa ujumla.


Aidha, mtoa mada katika sekta ya uchumi, Ndugu Rashidi Hassan Nakumbya, ameangazia maendeleo ya miundombinu na ustawi wa uchumi, akisema, “Tumepiga hatua kubwa sana katika Wilaya yetu. Tuna barabara nzuri, vijiji vyote vinafikika, na bei nzuri za mazao ni miongoni mwa mafanikio makubwa.”


Katika sekta ya afya, Bi Hawa Mpinga amebainisha mabadiliko makubwa tangu kipindi cha uhuru, akisema, “Kabla ya uhuru, akina mama walikuwa wanapoteza maisha kwa ukosefu wa huduma bora za afya. Leo tunajivunia hospitali kubwa na vituo vya afya vya kutosha. Magonjwa kama ukoma, ndui, na pepopunda ni hadithi sasa.”


Kwa upande wa ukatili wa kijinsia, Bi Lucia Chitanda ameeleza jinsi miaka 63 ya uhuru imeimarisha uhuru wa kijinsia, akisema, “Zamani wakoloni walitunyima fursa, lakini sasa ukatili unakemewa, taarifa zinatolewa kwa wakati, na wahusika wanachukuliwa hatua.”


Naye, Mama Magehema ameeleza mafanikio makubwa katika sekta ya elimu, akionesha tofauti kubwa iliyokuwepo kabla ya uhuru, baada ya uhuru, na hali ya sasa. Amepongeza juhudi za Serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu na mazingira bora ya kujifunzia ambayo yameongeza viwango vya ufaulu nchini


“Zamani, shule zilikuwa hazifaulishi kabisa. Ilikuwa kawaida kuona mtu mmoja au wawili tu wakifaulu, na ukikuta watatu ni bahati kubwa sana. Lakini siku hizi, ufaulu umeongezeka sana karibu darasa zima linafaulu. Kuna walimu wa kutosha, watoto wanafanya vizuri, na miundombinu imeboreshwa na ni rafiki sana kwa kujifunzia. Kwa kweli, tumepiga hatua kubwa,” amesema Mama Magehema.


Kongamano hilo limeonesha uzalendo na mshikamano miongoni mwa wananchi wa Ruangwa, huku likiwa na lengo la kutafakari mafanikio yaliyopatikana na kuhamasisha juhudi zaidi za maendeleo kwa miaka ijayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa