• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

RUANGWA WAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE ROBO YA NNE 2024/2025

Posted on: September 8th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, ameongoza kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe robo ya nne ya mwaka wa fedha 2024/2025 leo Septemba 08, 2025, kikilenga kujadili mafanikio, changamoto na kuweka mikakati mipya ya lishe.


Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kimehusisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, kamati ya ulinzi na usalama, wakuu wa idara na vitengo, watendaji wa kata, maafisa lishe wa kata zote pamoja na maafisa wa afya. Lengo kuu kimekuwa kutathmini utekelezaji wa shughuli za lishe kwa kipindi cha miezi mitatu, kuimarisha ushirikiano na kuhakikisha jamii inanufaika na huduma bora za lishe.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Ngoma amewapongeza watendaji wa kata zilizofanikisha viashiria vya lishe kwa kufikia malengo, amewataka waendelee kufanya kazi kwa bidii.

“Hongereni sana kwa kazi nzuri, mnajituma sana, nitumie nafasi hii kuwapongeza na kuwakumbusha kwamba kila kitu kinawezekana, fanyeni kazi kwa bidii na kwa kujituma, nategemea mwaka huu kata zote 22 zitafikia malengo kwa asilimia 100,” amesema Mhe. Ngoma.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Frank Fabian Chonya, amewataka watumishi wanaosimamia masuala ya lishe kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuhakikisha Ruangwa inakuwa ya kwanza kitaifa.


“Fanyeni kazi bila visingizio, tunao uwezo wa kufikia malengo kwa kila kata maana Serikali imeweka mazingira wezeshi, nategemea kuona tunavuka malengo kwa robo ya kwanza ya mwaka huu, kwa sasa tunaongaza kimkoa nataka tuongoze kitaifa” amesema Chonya.


Aidha, Mratibu wa Lishe wa Wilaya, Ndugu Barikieli Gulmay Duwe, ameeleza kuwa utekelezaji wa afua za lishe umejikita kwenye elimu mashuleni, usambazaji wa virutubisho na kampeni za uhamasishaji.


Washiriki wa kikao wamependekeza kuongeza kuwa juhudi ziongezwe kwa usimamizi wa karibu, ili kuimarisha utekelezaji na uboreshaji wa Lishe. Lakini pia, wameomba zoezi la kutoa elimu kwa wananchi liwe endelevu ili kuwajengea uelewa mkubwa zaidi.


Kikao kimehitimishwa kwa makubaliano ya kila sekta kutekeleza wajibu wake ipasavyo na kuimarisha ufuatiliaji katika mwaka wa fedha 2025/2026, huku wadau wakiahidi kushirikiana kwa karibu zaidi ili kuhakikisha malengo ya kitaifa ya lishe yanafikiwa kwa ufanisi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • BOT YAENDESHA SEMINA YA UWEKEZAJI HATI FUNGANI RUANGWA

    September 10, 2025
  • KILA LA HERI DARASA LA SABA KLATIKA MTIHAANI WENU WA TAIFA

    September 09, 2025
  • KILA LA HERI DARASA LA SABA KATIKA MTIHANI WENU WA TAIFA

    September 09, 2025
  • RUANGWA WAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA LISHE ROBO YA NNE 2024/2025

    September 08, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa