• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

RUANGWA WAFANYA KIKAO CHA MAABARA YA ELIMU

Posted on: December 2nd, 2024

Kikao cha Maabara ya Elimu ngazi ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kimefanyika leo, Desemba 2, 2024, katika bwalo la Shule ya Sekondari Ruangwa, kikilenga kuchambua changamoto, mafanikio, na mbinu bora za kuboresha sekta ya elimu.


Kikao hicho, ambacho kimeongozwa na Afisa Elimu Msingi wa Wilaya, Mwalimu George Mbesigwe, kimewakutanisha wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo Maafisa Elimu, wawakilishi wa Tume ya Utumishi wa Walimu, walimu wakuu, wakuu wa shule, na maafisa kutoka Idara ya Elimu, ajenda kuu zimehusu tathmini ya utekelezaji wa maazimio ya mwaka 2024, pamoja na mipango ya kuimarisha maendeleo ya sekta ya elimu wilayani.


Aidha, mada zilizojadiliwa ni pamoja na taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha maabara kwa mwaka huu, tathmini ya utekelezaji wa mpango mkakati, changamoto zinazokabili sekta ya elimu, mafanikio yaliyopatikana, na suluhisho za changamoto hizo, Zaidi ya hayo, kikao hicho kimeweka mkazo katika mafunzo endelevu kwa walimu ili kuwajengea uwezo zaidi wa kufanikisha malengo ya kielimu.


Vilevile, sehemu ya majadiliano imejikita pia katika utekelezaji wa shughuli za michezo, hususan mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA, ambayo yanatajwa kuchangia maendeleo ya wanafunzi kiakili, kimwili, na kijamii. Isitoshe, washiriki wamesisitiza umuhimu wa michezo shuleni kama sehemu ya kukuza vipaji na kuimarisha afya ya wanafunzi.


Hata hivyo, changamoto kama upungufu wa walimu na miundombinu duni bado ni vikwazo vilivyojadiliwa kwa kina. Akizungumza katika kikao hicho, Mwalimu George Mbesigwe amesema juhudi za pamoja kati ya walimu, wazazi, na Serikali zimekuwa na mchango mkubwa katika kuinua viwango vya elimu wilayani Ruangwa.


 “Lazima tuendelee kushirikiana kama jamii ili kuhakikisha tunapunguza changamoto na kuimarisha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wetu,” amesema Mbesigwe.


Kwa upande mwingine, wadau wa elimu wamekubaliana kuwa mpango mkakati wa elimu unapaswa kuzingatia vipaumbele vinavyolenga kuboresha miundombinu ya shule, kuongeza vifaa vya kujifunzia, na kushughulikia upungufu wa walimu. Kadhalika, wamesisitiza ushirikiano wa karibu kati ya shule na jamii ili kufanikisha malengo hayo.


Ikumbukwe, kikao hicho kinaonekana kuwa hatua muhimu katika kuhakikisha kuwa sekta ya elimu inapata msukumo mpya na kufanikisha maendeleo endelevu wilayani Ruangwa, washiriki wameonyesha matumaini kuwa utekelezaji wa maazimio ya kikao hicho utaleta matokeo chanya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa