• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA YATUNUKIWA TUZO KWA KUONGOZA KATIKA VIASHIRIA VYA AFYA MKOA WA LINDI

Posted on: May 3rd, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imetunukiwa tuzo maalum kwa kuongoza katika viashiria vya utekelezaji wa huduma za afya kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2025, miongoni mwa Halmashauri zote za Mkoa wa Lindi, tuzo hiyo imetolewa leo tarehe 3 Mei 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, katika kikao cha tathmini ya Kadi ya Utekelezaji wa Afya kilichofanyika wilayani Ruangwa.


Mafanikio haya yanaashiria hatua kubwa zilizopigwa na Halmashauri ya Ruangwa katika utoaji wa huduma bora za afya, ikiwa ni pamoja na huduma za mama na mtoto, matumizi ya mifumo ya kidijitali kama GoTHOMIS, usimamizi wa takwimu, na upatikanaji wa dawa muhimu.

Hali kadhalika, Kadi ya Utekelezaji wa Afya ni nyenzo ya kitaifa inayotumika kila robo mwaka kupima utendaji wa halmashauri kwa kutumia viashiria 42 kutoka katika maeneo 15 ya temati ya afya, ustawi wa jamii, na lishe. Viashiria hivi vinasaidia kutathmini hali ya utoaji wa huduma na ufanisi wa halmashauri.


Aidha, baadhi ya viashiria vya utekelezaji ni pamoja na: uzazi salama na chanjo, matumizi ya mifumo ya kidijitali ya afya (mfano GoTHOMIS), huduma za lishe, elimu ya afya kwa jamii, upimaji wa VVU na huduma za ARV, uwiano wa watumishi wa afya kwa idadi ya watu, pamoja na utoaji wa huduma kwa wakati na kwa ufanisi.


Kwa upande mwingine, mafanikio haya yasingewezekana bila uongozi thabiti na ushirikiano wa karibu kati ya viongozi wa kisiasa na wataalamu wa afya. Vilevile, juhudi za watumishi walioko mstari wa mbele katika vituo vya kutolea huduma zimechangia pakubwa katika kufanikisha utekelezaji wa huduma hizi.


Kwa ujumla, tuzo hii ni uthibitisho wa juhudi za pamoja katika kuboresha huduma za afya wilayani Ruangwa na kuonesha mfano mzuri kwa Halmashauri nyingine za Mkoa wa Lindi.


#RuangwaYetu

#AfyaBora

#TuzoYaUbora

#Lindi

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MPARA WAFANYA USAFI KUJIANDAA NA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU

    May 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA YATUNUKIWA TUZO KWA KUONGOZA KATIKA VIASHIRIA VYA AFYA MKOA WA LINDI

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa