• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Nielimishe Nikwamue Taifa Kiuchumi

Posted on: May 2nd, 2018

Wazazi Kutoka katika kata ya Chinongwe Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi watakiwa kuwapa nafasi watoto wao wa kike kusoma ili kupata elimu itakayowawezesha kulisaidia Taifa kukuza uchumi na kuboresha maisha yao ikiwa ni pamoja na kuzifikia ndoto zao.


Hayo yamesemwa  katika viwanja vya shule ya msingi Chinongwe kata ya Chinongwe WIlayani Ruangwa na Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Chinongwe Mwalimu Propronius Kashaija Rutazamba alipokua akizungumza katika Tamasha liloandaliwa la kumwelimisha mtoto wa kike kujitambua.


Aidha amesema mtoto wa kike akielimika ni sawa na kuielimisha jamii hivyo amehimiza wazazi kuwapa nafasi watoto wa kike wasome ili waweze kulisaidia Taifa katika kuongeza kasi ya maendeleo, huku akieleza pamoja na kuwa watalisaidia Taifa lakini hata wazazi wenyewe watanufaika na mafanikio hayo na kusema kuwa ni sehemu ya matunda watakayoyafurahia.

"Binti anapopata elimu ni tofauti kidogo na mtoto wa kiume, sisi wa kiume tukishapata elimu tukishatoka kwa mfano mm nimeshatoka inamaana mimi na familia yangu hao wazazi labda nitawarushia fedha kidogo lakini motto wa kike ndie anaetegemewa hasa katika familia” Alisema Mwalimu Propronius.

Katika hatua hiyo nae Mwalimu Zaudia Juma manzi wa shule ya msingi Likunja aliefika katika Tamasha hilo kama shuhuda wa kuelezea safari yake ya mafanikio, amewataka wanafunzi kutokukatamaa kwani hata yeye alipitia majaribu na misukosuko katika wakati wake wa masomo lakini aliidhibiti na kusimamia kukamilika kwa ndoto zake na mpka sasa amefanikiwa kupata kazi ya ualimu na sasa anafurahia maisha kw kukamilisha ndoto zake.

“Kwahiyo jamani watoto wa kike tubadilike na tuipende shule ili tufikie sehemu nzuri tunazotamani kufika kwa mujibu wa ndoto zetu” Alisema Afisa Elimu kata ya Chinongwe Mwalimu Abdallah Omari Njarimbo anaelezea kufanikiwa kwa kongamo hilo huku akieleza jumla ya wasichana 951 kutoka shule za msingi Juhudi, Chinongwe, Litama na Likwachu wamepatiwa elimu hiyo na kusema kuwa anamini kutatokea mabadiliko makubwa katika kata hiyo.

Wakati huo huo wanafunzi walioshiriki kongamano hilo lililolenga kumuelimisha mototo wa kike kujikomboa Amina Rashidi Bakari wa shule ya msingi Juhudi na Martha Athumani wa shule ya msingi Chinongwe, wanaelezwa juu ya manufaa waliyoyapata kwenye tamasha hilo kuwa ni pamoja na kuhamisika juu ya kupenda elimu lakini kubwa kukamilisha kwa ndoto zao hasa kutoa mfano walioupata kwa mgeni mwalikwa na hivyo kuahidi kusoma kwa bidii ili kuyafikia malengo yao.

Hatua hii ya kongamano la kumuelimisha mtoto wa kike apate elimu ya kujitambua inakuja katika Kata hiyi ikiwa siku za hivi karibuni kuonekana ufaulu wa mtoto wa kike kushuka na kusababisha kuwa na matokeo mabaya hivyo viongozi wa elimu kata chinongwe kuona haja ya kutoa elimu na hamasa ili kuwatia moyo wanafunzi hao waweze kuongeza juhudi katika masomo yao.


Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • TAARIFA KWA UMMA

    June 04, 2025
  • WANAFUNZI RUANGWA WAIBUKA KIDEDEA USAFI NA UNADHIFU UMISSETA 2025 MKOA WA LINDI

    June 01, 2025
  • MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MRADI WA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA NISHATI SAFI WANDORWA

    May 28, 2025
  • RUANGWA YAPOKEA MWENGE WA UHURU 2025 KUTOKA LINDI MANISPAA

    May 28, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa