• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

NANDAGALA MARATHON YAANDIKA HISTORIA WILAYANI RUANGWA

Posted on: September 28th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nandagala, Mhe. Andrew Chikongwe, ameeleza kuwa mbio za Nandagala Marathon zimeweka historia kwa kuwa ni za kwanza kufanyika katika ngazi ya kata katika Wilaya Ruangwa. 


Akizungumza leo Septemba 28, 2024, katika viwanja vya Stendi Nandagala, Mhe. Chikongwe amesema,

 "Kwa kawaida, Marathon hizi hufanyika katika ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa, lakini kwa ngazi ya Kata, hii ni ya kwanza kufanyika wilayani Ruangwa na kanda yote ya Kusini." Ameongeza kuwa tukio hilo limeonesha mwelekeo mpya katika kukuza michezo na kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki shughuli za maendeleo.


Mbio hizo zimehusisha washiriki kutoka Wilaya za Ruangwa, Nachingwea, na Liwale, ambapo waneshindana katika mbio za kilomita 21, kilomita 10, kilomita 5, na kilomita 3 kwa wanafunzi wa shule za msingi, Washindi wa kila kundi wamejinyakulia zawadi nono, hali iliyoongeza msisimko na hamasa miongoni mwa washiriki na watazamaji.


Aidha, Mhe. Chikongwe ametumia fursa hiyo kuipongeza Redio Jamii ya Ruangwa, Ruangwa FM, kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha mbio hizo. "Nawashukuru sana Ruangwa FM, wamejitoa kwa nguvu zao zote kuhakikisha Nandagala Marathon inafanikiwa, bila shaka wamefanya kazi kubwa ya kulipa hadhi tukio hili," amesema Mhe. Chikongwe


Sambamba na pongezi hizo, Mhe. Chikongwe pia ametoa wito kwa wadau mbalimbali na wananchi kuendelea kushirikiana katika shughuli za maendeleo, siyo tu ngazi ya kata bali pia Wilaya na Mkoa kwa ujumla, amesema mshikamano huu unapaswa kuendelezwa katika sekta nyingine ili kuleta ustawi wa jamii.


NANDAGALA MARATHON:

HALI YA ZAMANI, SASA NA MUSTAKABALI.

Zamani, matukio makubwa ya michezo kama marathon yalikuwa nadra kufanyika ngazi ya kata wilayani Ruangwa, hali iliyosababisha wananchi wengi kukosa fursa ya kushiriki kwenye mashindano hayo. Hata hivyo, tukio hili la kwanza katika Kata ya Nandagala linaashiria mwanzo mpya, ambapo michezo inaweza kuwa kiungo muhimu cha umoja na maendeleo katika jamii.


Kwa sasa, mbio hizi zimeonyesha kuwa michezo inaweza kuhamasisha ushiriki mkubwa wa wananchi, si tu kama washiriki bali pia wadau wa maendeleo. Washindi wa mbio hizi, pamoja na kupata zawadi, wameonesha mfano wa kuigwa kwa kujitoa na kuchangia maendeleo ya kijamii kupitia michezo.


Kwa siku zijazo, kuna haja ya kuimarisha ushirikiano baina ya wadau mbalimbali ili kuhakikisha mbio kama hizi zinafanyika mara kwa mara, si tu katika kata bali pia katika Vijiji na Wilaya nzima kwa ujumla. Hii itasaidia kuongeza kasi ya maendeleo ya michezo na kuleta fursa mpya kwa vijana na jamii kwa ujumla. Serikali na sekta binafsi zinapaswa kuendelea kutoa msaada wa vifaa, rasilimali, na motisha kwa washiriki na waandaaji wa matukio kama haya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa