• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA AWATAKA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WA KIKE WANALINDWA NA KUPATA ELIMU BORA

Posted on: October 31st, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Andrew Chikongwe, ametoa rai kwa wazazi, walezi, na jamii kwa ujumla kuhakikisha watoto wa kike wanalindwa na wanapewa elimu bora pamoja na matunzo wanayostahili, hayo yamesemwa jana, Oktoba 30, 2024, katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani ambapo wilayani Ruangwa yamefanyika kata ya Nandagala.


Mhe. Chikongwe, ambaye amekuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, ametoa rai kwa wazazi, walezi, na jamii kwa ujumla kuhakikisha watoto wa kike wanalindwa na wanapewa elimu bora pamoja na matunzo wanayostahili.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwa na mazingira salama kwa watoto wa kike ili waweze kukua na kutimiza ndoto zao. 


“Katika dunia ya sasa kuna watu wema lakini pia wapo wabaya wanaoweza kuharibu maisha ya watoto wetu,” amesema Chikongwe, akihimiza wazazi kuwapa watoto nafasi ya kuzungumza kwa uwazi bila woga.


Sambamba na hayo, amewahimiza walimu kuendelea kuwalea watoto katika maadili mema na kuwa na mtazamo chanya kuhusu maisha. 


“Walimu tunawaomba muendelee kutulelea watoto wetu kwenye maadili mwema,” ameongeza.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Child Welfare ameushukuru uongozi wa Wilaya ya Ruangwa kwa ushirikiano na mapokezi mazuri waliouonyesha katika kufanikisha maadhimisho hayo.


Maadhimisho hayo yamelenga kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa kulinda haki za mtoto wa kike na kumwezesha kupata fursa sawa na kujijengea mustakabali bora. Siku hiyo pia imetumika kuwaelimisha wazazi na walezi kuhusu wajibu wao katika kuhakikisha watoto wa kike wanapata haki ya elimu, ulinzi, na malezi bora. Viongozi na wadau wametoa shukrani kwa juhudi za wilaya hiyo kuendeleza ustawi wa watoto wa kike na kuihimiza jamii kushirikiana katika kujenga msingi imara kwa kizazi kijacho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa