• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MWENYEKI WA HALMASHAURI AHIMIZA WATENDAJI KATA KUWA MABALOZI WA KILIMO CHA KISASA

Posted on: September 17th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Andrew Chikongwe, amewahimiza watendaji wa Kata kuwa mabalozi wa kilimo cha kisasa kwa kuonesha mfano wa vitendo, akizungumza katika semina maalum ya tathmini na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo iliyofanyika leo, Septemba 17, 2024, katika Shule ya Sekondari Ruangwa, Mhe. Chikongwe amewataka watendaji wa Kata kuhakikisha kwamba wanatekeleza kilimo cha kisasa kwa kutumia mbolea bora na mbinu za kisasa, na hivyo  kuwa mifano hai kwa wananchi wa Wilaya ya Ruangwa.


Mhe. Chikongwe amesisitiza kuwa Watendaji wanapaswa kuonesha kwa vitendo matumizi ya teknolojia ya kisasa na kutoa mfano wa jinsi ya kupanda mazao bora ili kuvutia na kuhamasisha wananchi. Ameongeza kuwa, watendaji wakishiriki moja kwa moja katika kilimo cha kisasa kutasaidia kuongeza uelewa na kuhamasisha wakulima kuiga mifano yao.


Aidha, Mhe. Chikongwe ameongeza kuwa lengo kuu la juhudi hizi ni kuifanya Wilaya ya Ruangwa kuwa kinara wa kilimo nchini.  Watendaji wakiwasaidia wananchi kwa vitendo, wataongeza ufanisi wa kilimo na kuboresha uzalishaji, na hivyo kusaidia Wilaya kuwa kitovu cha utalii na uwekezaji katika sekta ya kilimo.


Ameongezea kwa kusema “hali ya kilimo katika Wilaya ya Ruangwa imekuwa ya tofauti kutokana na jitihada mpya zinazofanywa na Serikali, ikiwa ni pamoja na kupeleka pembejeo za kutosha maeneo yote, hivyo basi kuna matumaini ya kuona mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo. Wataalamu wa kilimo wanapaswa kuendelea kutoa elimu kwa wakulima na kuwa sehemu ya utekelezaji wa mbinu bora za kilimo ili kuhakikisha kwamba mikakati ya kilimo inatekelezwa kwa ufanisi” amesema Mhe. Chikongwe.


Ikumbukwe, Kwa kuzingatia mifano bora na kuhakikisha kwamba wakulima wanapata mafunzo sahihi na vifaa vya kisasa, Wilaya ya Ruangwa inaweza kufikia malengo yake ya kuwa kiongozi katika kilimo. Ili kufanikisha hilo, ni muhimu kuendelea kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa wakulima, huku ikifanyika kazi kwa ukaribu na wataalamu wa kilimo na wadau wengine, hii itasaidia kuimarisha kilimo bora na kuhakikisha kuwa Ruangwa inakuwa mfano wa kuigwa katika kilimo cha kisasa nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa