Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2025, ukiongozwa na Comrade Ismail Ussi, leo Mei 28, umetembelea na kukagua Mradi wa Uhifadhi wa Mazingira na Utumiaji wa Nishati Safi na Salama unaotekelezwa na kikundi cha Mama Lishe WANDORWA katika Wilaya ya Ruangwa, ambapo viongozi wa mbio hizo wameonesha kuridhishwa na utekelezaji wake.
Mradi huo unalenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi kama majiko banifu na gesi asilia kwa vikundi vya wanawake wanaojishughulisha na shughuli za upishi, ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa ambayo ni chanzo kikuu cha uharibifu wa mazingira.
Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Comrade Ismail Ussi, amesema kuwa mradi huo ni mfano wa ubunifu unaoendana na ajenda ya taifa ya kuhifadhi mazingira na kuimarisha afya ya wananchi kupitia matumizi ya nishati mbadala.
“Mradi huu umeonesha namna wanawake wanavyoweza kuwa chachu ya mabadiliko ya kimazingira na kiafya kwa jamii. Tunapongeza juhudi hizi ambazo pia zinatoa fursa za kiuchumi kwa wanawake,” amesema Comrade Ussi.
Aidha, Mwenge wa Uhuru 2025 unaendelea kutoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu ujao kwa njia ya amani na utulivu, ili kulinda mafanikio ya maendeleo kama haya.
Ruangwa
Anuani ya Posta: S.L.P 51
Simu ya Mkononi: 0732932312
simu: 0732932312
Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa