• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA YA RUANGWA AZINDUA ZOEZI LA KUWEKA VIFARANGA VYA SAMAKI KATIKA MABWAWA MANDAWA

Posted on: October 29th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, leo Octoba 29, 2024 amezindua rasmi zoezi la uwekaji wa vifaranga vya samaki katika mabwawa yaliyopo Kijiji cha Nahanga, Kata ya Mandawa, wilayani Ruangwa, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, ambaye alitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika zoezi hilo ambalo jumla ya vifaranga 7,000 vimepandikizwa kwenye mabwawa hayo, ikilinganishwa na lengo lililokusudiwa la kupandikiza vifaranga 6,000, ambapo vifaranga 1,000 vya ziada vimewekwa ili kufidia upotevu unaoweza kutokea.


Mhe. Ngoma amepongeza juhudi za Serikali katika kuanzisha mradi huo muhimu, ambao unalenga kuongeza kipato na fursa za ajira kwa jamii ya Ruangwa, na ameeleza kuwa mradi huo utakuwa kichocheo muhimu cha maendeleo katika sekta ya uvuvi wilayani humo.


Aidha, kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndg. Radhidi Namkulala, ameishukuru Serikali kwa kuleta mradi huo na kuahidi kuhakikisha mradi unalindwa na kuleta matokeo yanayotarajiwa. 

“Tunashukuru sana kwa mradi huu wa kimkakati, tutaulinda na kuhakikisha unazaa matunda kama ilivyokusudiwa,” amesema Namkulala.


Naye mwakilishi kutoka Wizara ya Uvuvi, Ndg. John Malya, amesisitiza umuhimu wa kufuata maelekezo ya wizara kwa wanakikundi wanaosimamia mradi huo, akisisitiza kuwa ni muhimu kuzingatia miongozo yote ili kufanikisha mradi kwa asilimia 100.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ruangwa, Mhe. Andrew Chikongwe, ameipongeza Serikali kwa mradi huo wa ufugaji wa samaki na kusema kuwa ni fursa adhimu kwa wakazi wa Ruangwa kujifunza na kukuza uchumi. 

“Mradi huu ni darasa muhimu sana kwa wafugaji wa samaki, tunashukuru sana kwa fursa hii, wanamandawa na wanaruangwa kwa ujumla tuutunze mradi huu wenye uwekezaji wa thamani kubwa sana” amesema Chikongwe.


Naye, Diwani wa Kata ya Mandawa, Mhe. Rashid Lipei, amewahimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika kutunza mradi huo na kuhakikisha unakuwa endelevu kwa manufaa ya kizazi kijacho.


Hata hivyo, Wananchi wa Kata ya Mandawa, wakiongozwa na Bi. Asha Issa, wameeleza furaha yao kwa mradi huo, wakisema ni fursa adimu kwao kupata ujuzi na kuboresha maisha yao. 

“Mradi huu umetuongezea matumaini na tumefurahia sana, tutaushika vizuri kama tulivyoelekezwa,” amesema Bi. Asha.


Ikumbukwe, mradi huo wa mabwawa ya ufugaji wa samaki ni moja ya uwekezaji wa Serikali unaolenga kuboresha sekta ya uvuvi nchini na kuinua maisha ya wananchi kwa kuwawezesha kujipatia kipato kupitia ufugaji endelevu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa