• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA YA RUANGWA AHIMIZA USHIRIKISHWAJI WA JAMII KATIKA SEKTA YA UCHIMBAJI

Posted on: September 26th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, leo Septemba 26, 2025 ameshiriki mafunzo ya Extractive Baraza yaliyoandaliwa na taasisi ya HakiRasilimali katika Hotel ya Ruangwa Pride, akisisitiza ushirikishwaji wa jamii na wadau katika sekta ya uchimbaji madini.


Mafunzo hayo yamewaleta pamoja wanajamii, wadau wa maendeleo na viongozi wa eneo hilo ili kujadili fursa na changamoto za sekta ya uchimbaji. Aidha, washiriki wamepata nafasi ya kuangazia namna rasilimali zinavyoweza kutumika kwa faida ya wote, pamoja na mbinu za kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika matumizi ya mapato yatokanayo na uchimbaji.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mhe. Ngoma, amesema ushiriki wake unaashiria dhamira ya Serikali ya kusikiliza wananchi na kushirikiana nao katika kupanga maendeleo. 

“Serikali inataka kuona kila mwananchi anapata nafasi ya kushiriki, kutoa maoni na kueleza matarajio yake kuhusu sekta ya uchimbaji, sekta hii ina fursa kubwa na manufaa yake yanapaswa kuwafikia wananchi wote kwa usawa”. amesema Mhe. Ngoma.


Zaidi ya hayo, washiriki wamejadili namna sekta ya uchimbaji inaweza kuwa kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kushirikisha makundi yote, hususan vijana na wanawake. Wameona kuwa ushiriki wa makundi hayo ni msingi wa kuleta ustawi wa jamii kwa usawa na kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika maendeleo.

Hata hivyo, baraza limeweka msisitizo katika mshikamano kati ya jamii na wadau kwa kusisitiza kuwa uwazi wa taarifa ni chachu ya kuimarisha imani na ushirikiano. Lakini pia, Washiriki wamekubaliana kuwa utaratibu wa kutoa taarifa wazi kuhusu mapato na matumizi ya sekta ya uchimbaji utasaidia kujenga uwajibikaji wa pamoja na kuimarisha maendeleo ya muda mrefu.


Halikadhalika, changamoto zinazojitokeza katika maeneo ya uwekezaji wa uchimbaji, ikiwemo athari za kimazingira, ajira na uhusiano wa kijamii, zimejadiliwa kwa kina. Washiriki wamesema kuwa majadiliano ya aina hii ni jukwaa muhimu la kutafuta suluhu za pamoja zinazojenga uelewano kati ya wananchi na wawekezaji.


 Akizungumza kwa niaba ya washiriki wengine Mohamedi Chilemba amesema, wanaishikuru taasisi ya Hakirasilimali kwani mafunzo hayo yamewajengea uwelewa mpana kuhusu Sekta ya uchimbaji akisisitiza kwamba mshikamano wa jamii ndio msingi wa maendeleo endelevu.

“Kauli mbiu yetu katika mafunzo haya imebeba maana kubwa tunawashukuru sana wawezeshaji wetu tumejifunza mengi kikubwa siku zote nitaishika kauli mbiu ya mafunzo haya isemayo “A community that speaks together, grows together” ikimaanisha mshirikiano wa jamii ndio njia ya kuleta maendeleo jumuishi na ya kudumu. Amesema” Mohamedi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • ZIMESALIA SIKU 16 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 13, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 18 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 11, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 23 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 06, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 24 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 05, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa