• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKURUGENZI CHONYA AKAGUA UJENZI WA HOSTELI ZA NAMUNGO FC, ATOA MAELEKEZO YA KUKAMILISHA KABLA YA AGOSTI KUISHA

Posted on: July 31st, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Frank Fabian Chonya, amefanya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa hosteli za timu ya Namungo FC na kutoa agizo la kuhakikisha kazi hiyo inakamilika mwishoni mwa mwezi Agosti 2025.


Katika ziara hiyo ya ukaguzi iliyofanyika leo tarehe 31 Julai 2025, Mkurugenzi Chonya ameambatana na Wakuu wa Idara, Vitengo pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka Halmashauri hiyo kwa lengo la kujiridhisha na hatua ya utekelezaji wa mradi huo muhimu kwa maendeleo ya michezo.


Akizungumza mara baada ya ukaguzi, Mkurugenzi Chonya amesema ni muhimu hosteli hizo zikakamilika kwa wakati ili kuwapa wachezaji wa Namungo FC mazingira bora ya kujiandaa kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya NBC. Amesisitiza kuwa timu hiyo inapaswa kuhamia rasmi katika hosteli hizo mapema mwanzoni mwa msimu wa ligi.

“Tunataka Namungo FC iwe na mazingira bora ya kambi, ili iweze kujiandaa kikamilifu na kufanya vizuri zaidi kwenye ligi, amesema Chonya.

Aidha, ameelekeza wakandarasi kuongeza kasi ya kazi na kuhakikisha viwango vya ubora vinafuatwa, huku akiwataka wasimamizi wa mradi kufuatilia kwa karibu kila hatua ya utekelezaji ili kuepuka ucheleweshaji usio wa lazima.


Zaidi ya hayo, Mkurugenzi ameeleza dhamira ya Serikali ya Wilaya ya Ruangwa ya kuendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya michezo, hasa kwa timu zinazowakilisha Wilaya katika mashindano ya kitaifa, ili kukuza vipaji na kuinua jina la Ruangwa kimichezo.


Vilevile, viongozi na wataalamu walioambatana naye wameahidi kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano ili kuhakikisha  ujenzi wa hosteli hizo unakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.


Kwa ujumla, mradi wa hosteli za Namungo FC ni sehemu ya jitihada za Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa katika kuimarisha mazingira ya michezo na kuwawezesha wanamichezo wa ndani kupata nafasi ya kushindana katika viwango vya juu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI CHONYA AKAGUA UJENZI WA HOSTELI ZA NAMUNGO FC, ATOA MAELEKEZO YA KUKAMILISHA KABLA YA AGOSTI KUISHA

    July 31, 2025
  • WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI MWAKA 2025 KUAANZA KESHO

    July 31, 2025
  • MKURUGENZI RUANGWA AZINDUA JARIDA LA AFYA KUHAMASISHA HUDUMA BORA

    July 28, 2025
  • ASHALONGO FC YAIBUKA KIDEDEA KWA PENALTI 6:5 DHIDI YA TIMU YA AFYA, YANYAKUA MBUZI MAJALIWA STADIUM

    July 27, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa