• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKURUGENZI CHONYA AKABIDHIWA VIFAA VYA TEHAMA KWA AJILI YA SHULE ZA SEKONDARI RUANGWA

Posted on: July 6th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Ndugu Frank Fabian Chonya amekabidhiwa vifaa vya TEHAMA na Kampuni ya Reneal International Education Outreach chini ya Mkurugenzi Ndugu David Nyangaka zitakazotumika katika shule za Sekondari wilayani Ruangwa.


Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo Julai 6, 2024 na Juma Mshihiri ambaye ni fundi wa vifaa vya TEHAMA kwa niaba ya Mkurugenzi wa Kampuni hiyo.


Aidha, vifaa hivyo ni pamoja na Komputa mpakato (Laptop) 100, Vihifadhia nukuu na vifaa vya kujifunzia (Server) 5, vifaa vya kutunza umeme (UPS) 5, na vifaa vya kudhibiti umeme (Regulator) 5.


Shule zilizokabidhiwa vifaa vya TEHAMA ni tano zenye kidato cha tano na sita kwa Wilaya ya Ruangwa, ambazo ni shule ya Sekondari Hawa Mchopa, Lucas Malia, Nkowe, Ruangwa na Mbekenyera.


Katika hatua nyingine, Ndugu Frank Fabian Chonya amewataka Wakuu wa shule hizo kujenga vizuri vyumba maalumu kwa ajili ya matumizi ya komputa mpakato hizo ili wanafunzi waweze kuvutiwa kuingia kujisomea.


Aidha, Ndugu Chonya amesisitiza kwa kusema kuwa komputa mpakato hizo zitumike vizuri na zitunzwe ipasavyo ili ziweze kupandisha ufaulu wa wanafunzi katika Wilaya ya Ruangwa.


"Kwa msaada wa hizi Laptop, Ruangwa sasa tunaenda kuwa namba moja kitaifa kwa ufaulu wa Kidato cha sita" amesema Chonya.


Naye, Mkuu wa shule ya Sekondari Lucas Malia Gladness Makongwa kwa niaba ya Wakuu wa shule za Sekondari zilizonufaika na vifaa hivyo vya TEHAMA ameishukuru Kampuni ya Reneal International Education Outreach kwa msaada huo na kumuahidi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kuyatekeleza yale yote aliyoyaagiza kwao ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MPARA WAFANYA USAFI KUJIANDAA NA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU

    May 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA YATUNUKIWA TUZO KWA KUONGOZA KATIKA VIASHIRIA VYA AFYA MKOA WA LINDI

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa