• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Millioni 61 kuwafaidisha Wanawake, Vijana na Walemavu Ruangwa

Posted on: July 24th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imetoa shilingi millioni 61 kwa ajili ya  mikopo ya vijana, wanawake na walemavu kwa vikundi 28 vilivyopo Wilayani humo.

Hayo yamesemwa leo 24/07/2019 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo alipokuwa akiongea na wanavikundi hao  katika ukumbi wa Rutesco mjini Ruangwa

katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa ndg, Andrea Chezue alisema huo siyo mwisho wa wanavikundi kupata mikopo hiyo, mwezi wa 8 mwaka huu Halmashauri itatoa million 100 kwa wanavikundi watakaoomba.



"Rudisheni kwa wakati marejesho yanayotakiwa muombe tena kwani fedha ziko za kutosha na zipo kwa ajili yenu ombeni kwa kufuata utaratibu mliowekewa nawahakikishi mtapata mikopo hiyo"

Ndg, Chezue alisema Halmashauri inaangalia uwezekano wa kuongeza fedha kwenye fungu la wanawake kwasababu wamekuwa wanarudisha kwa wakati marejesho yao na kundi lao limekuwa na uhitaji mkubwa kuliko makundi mengine.

Pia amewataka maafisa maendeleo ya kata na vijiji kuhamasisha watu wenye ulemavu kuunda vikundi vya ujasiliamali Ili waweze kujipatia mikopo ambayo inatengwa kwa ajili yao


"Sijafurahishwa na idadi ya kundi la watu wenye ulemavu ni vikundi vitatu tu ambayo vimepata fedha katika hiyo Milion 61 jitahidi sana huko kwenye kata na vijiji kutoa elimu kwa kundi hili wajue umuhimu wa hivi vikundi"

Aidha aliwatahadharisha wanavikundi wanaosubiri wagawane fedha alafu wavunje kikundi safari hii kutakuwa na ukaguzi wa kila baada ya mwezi 1, wataalamu wa Halmashauri watakuwa wanapitia kuangalia maendeleo ya kikundi hiko.


Alisema Mkurugenzi Chezue kikundi kinachoundwa na kinachosajiliwa kisife tunataka idadi ya watu waongezeke na si wapungue kikundi kitakachokiuka jambo hili kitajipunguzia nafasi ya kupata tena mkopo.

Ndg, Chezue aliwasisitiza wanavikundi kuanzisha  viwanda vidogo vidogo na kuwaahidi kuwawezesha watakao fanya mchakato huo.

Sambamba na hayo aliwahamasisha Wanawake kuchukua fomu za uchaguzi wa serikali za mitaa unaokaribia kutokana na wanawake kuwa makini katika mambo yao yote.


"Siyo kwamba kinababa hamko makini hapana mko makini pia ila kinamama nawao wachukie nafasi katika serikali za vijiji na kata ili kuwe na usawa wa majukumu kwa wanawake kwani wanaweza sana tu"


Naye bi, Emelda Chiwemba aliyeongea kwa niaba ya wanavikundi aliishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kuweza kuwapatia  mikopo hiyo na pia aliwataka wanavikundi kuwa wabunifu zaidi na kuongeza ujuzi kupitia vikundi vingine.



Alisema bi, Emelda kusingekuwepo na huo utaratibu wa kukopeshwa na Halmashauri watu wengi wasingeweza kufanikiwa kama walivyofanikiwa sasa mikopo hiyo imetuinua zaidi.

"Mkurugenzi Chezue naomba nikuhakikishie tunaahidi kurejesha kwa wakati marejesho tunayotakiwa, nakuahidi hayatosua sua, kila mtu anataka arudishe apate nyingine kwa hili hatutokuangusha"


Pia amewataka wanakikundi  kujifunza kupitia vikundi vingine ili waongeza ujuzi  kufikia malengo ya kuwa na viwanda vidogo vidogo.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa