• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Million 55 Zatolewa kwa VIjana na Wanawake Wajasilimali Ruangwa

Posted on: April 21st, 2018

Halmashauri ya WIlaya Ruangwa Mkoani Lindi kupitia Idara yake ya Maendeleo ya Jamii imetoa tsh milioni hamsini na tano laki tatu na elfu hamsini (55,350,000/=) kuwakopesha vikundi vya vijana na wanawake wajasiliamali WIlayani humo kwa lengo la kuwakwamua kiuchumi.


Akizungumza katika ukumbi wa Rutesco WIlayani humo, kabla ya kukabdhi hundi hiyo kwa vikundi vya wajasiliamali, Mkuu wa Wilaya Ruangwa mh. Joseph Mkirikiti, amesema, pesa hizo zinatolewa ili jamii iweze kukuza uchumi na hivyo ni lazima kuzingatia masharti ikiwamo pamoja na kurudisha kwa wakati ili vikundi vingine viweze kupata nafasi ya kukopa .


Aidha amekemea juu ya tabia za watu wasioaminika kuchukua mkopo na kukwama kurudisha kwa wakati kuwa haifai kuwaacha na badala yake ameitaka Idara ya Maendeleo ya Jamii Wilayani humo kuwaelimisha wana vikundi vya ujasiliamali ili waweze kujua umuhimu wa kutumia fursa hiyo na kurudisha mkopo kwa wakati.


“Mnapochaguana chaguaneni watu mnaojuana vizuri, watu wasioaminika epukaneni nao, mikopo ni lazima irejeshwe na Yule asiekopesheka asikopeshwe” alisema Mkirikiti

Afisa Maendeleo ya jamii Wilayani Ruangwa bw. Rashidi Namkulala , amesema lengo kuu la kutoa mikopo hiyo ni kuwawezesha wajasiliamali  waweze kuendesha shughuli zao wanazozifanya ili kuongeza kipato, huku akieleza kuwa mikopo hiyo imetokana na asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri inayotengwa kutoka kwenye vyanzo mbali mbali kwa ajili ya kuwawezesha vikundi vya wajasiliamali.


Amesema hii ni awamu ya kwanza na kuwa awamu nyingine wanataegemea kutoa mikopo mwezi Mei na tayari vikundi vya wajasiliamali vimeshatuma maombi ya kutaka mikopo kupitia ofisi hiyo ya maendeleo ya jamii ambapo, wanategemea kuwapatatiwa mikopo hiyo mara baada ya utaratibu kukamilisha.

“Mpaka sasa hivi tumepokea maombi mengine ya vikundi ambayo imeomba mikopo mbayo tunatarajia mpka mwisho wa mwezi wa Mei tuwagawie hivyo vikundi vingine ambao wameomba mikopo” alisema Rashidi, ambae ni afisa maendeleo ya jamii WIlayani Ruangwa.

Nao wajasiliamali ambao ni wanufaika wa mkopo huo wameishukuru Halmashauri ya WIlaya Ruangwa kwa kuwawezesha kuwapatia mikopo hiyo huku wakiahidi kutumia kwa usahihi na kurudisha kwa wakati ili kutoa fursa kwa vikundi vingine kukopa na kujikwamua kiuchumi.


Anusiata Cosmas ambae ni mjasiliamali kutokea kijiji cha Nandanga  amesema kupatikana kwa mikopo hiyo ni nusura kwa vikundi vya wajasiliamali hivyo ni vyema kuitumia fursa hiyo vizuri huku akisisitiza kuwa kila mmoja anajua jinsi hali ya kiuchumi ilivyokua ngumu na hivyo unapopata fursa ni vizuri kuheshimu na kuitumia kama inavyopaswa.


“Tunashukuru sana Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, kwa kutupatia huu mkopo, huu mkopo utaenda kutusaidia zaidi kutuinua kiuchumi, maana hali ilikua sio nzuri kidogo kiuchumi lakini huu mkopo utaenda kutuwezesha kutuinua kidogo maana kuna miradi mingi ambayo tumeianzisha kma vile bustani, na kazi za ujasiliamali wa mikono”. Alisema anusiata.


Jumla ya vikundi 32 ambavyo 21 ni vikundi vya wanawake, vikundi 10 ni vijana na kikundi 1 ni walemavu, wanaojishughulisha na shughuli za ujasiliamali wa utengenezaji bidhaa, kama batiki, sabuni, vibegi, kulima bustani na mama lishe, wamepatiwa mkopo wilayani humo, ambapo kwa mujibu wa maelezo ya afisa wa maendeleo ya jamii wilayani ruangwa vikundi vingine vinavyoendelea kuomba mikopo hiyo watapatiwa mkopo mwezi wa tano mwaka huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa