• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MHE. TELACK AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA.

Posted on: November 6th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack leo, Novemba 06, 2025 ameongoza kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe na Afua za Lishe Mkoa kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Juni 2025 kilichofanyika katika Ukumbi mkubwa wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.


Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhe. Telack amewataka viongozi na watendaji wote kuhakikisha wanasimamia ipasavyo utekelezaji wa shughuli za lishe katika maeneo yao sambamba na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu lishe bora ili kujenga jamii yenye afya.


“Lishe ni kipaumbele, Lishe ni chakula ni dawa, mwili wako ni kile unachokula. Hakikisheni fedha za lishe zinatoka kwa wakati na zinatumika kama ilivyokusudiwa. Kina baba na mama wajawazito wahimizwe kwenda kliniki pamoja ili kubaini mapema changamoto za upungufu wa damu na lishe na waweze kupata njia za kukabiliana nazo kwa pamoja ili kuimarisha afya ya mama kipindi cha ujauzito na mtoto anayetarajiwa kuzaliwa” amesisitiza.


Aidha, Mhe. Telack amesisitiza umuhimu wa kuimarisha sekta ya kilimo kupitia mashamba darasa kuanzia ngazi ya kijiji hadi kata, ili kutoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya uzalishaji wa mazao ya chakula na bustani ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.


Vilevile,amewahimiza Maafisa Elimu kuhakikisha shule zote zinatenga maeneo ya wanafunzi kujifunzia kazi za mikono ikiwemo kilimo cha mazao mbalimbali ikiwemo ya chakula ili watoto wapate chakula cha mchana na kujifunza kazi za mikono na kueleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuandaa kizazi kinachowajibika na kinachothamini kilimo.


“Niwaombe sana kila mmoja kwenye nafasi yake asimamie vizuri ili tuweze kwenda sambamba. Kila mmoja akisimama vizuri tunaamini scorecard zetu zitakuwa kijani. Twende tukajenge lishe za wananchi wetu ili kupunguza sababu za wananchi kwenda hospitali mara kwa mara bila sababu za msingi,” ameeleza.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa Bi. Zuwena Omary amesisitiza uanzishwaji na ufuatiliaji wa mashamba darasa kuanzia ngazi za vijiji na kata ili kutoa fursa kwa wananchi kujifunza namna ya uzalishaji bora wa mazao ya chakula na bustani kwa tija ya kuongeza upatikanaji wa chakula na kuimarisha afya za wanajamii.

Afisa Lishe wa Mkoa Bi. Juliana Chikoti ameeleza kuwa kwa mwaka 2024/25 Mkoa umefanikiwa kutumia fedha kiasi cha shilingi milioni 311 kati ya milioni 376 zilizotengwa kwa ajiri ya kuratibu shughuki za huduma za lishe sawa na 86% na kubainisha changamoto kuu zinazokabili sekta hiyo ni pamoja na utoaji wa fedha za Lishe kwa wakati, ongezeko la watoto wanaozaliwa na uzito pungufu, upungufu wa unga wenye virutubisho, na idadi ndogo ya watoto wanaopata chakula shuleni.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • MHE. TELACK AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA.

    November 06, 2025
  • MAAFISA LISHE WATOA ELIMU KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA

    November 06, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI

    November 04, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA RUANGWA ASHIRIKI KUPIGA KURA KITUO CHA RUTESCO

    October 29, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa