• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Mhe, Ndemanga Awataka Waendesha Pikipiki Kujifunza Alama za Barabarani Ili Kupunguza Ajali Za Barabarani.

Posted on: November 24th, 2017

 Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe, Shaibu Ndemanga aliyekuwa anamuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Nenda Kwa Usalama Barabarani, amewataka waendesha Pikipiki kujifunza alama za barabarani kwa umakini na kuzitumia kama ambavyo zinaelekezwa.

 

Mhe, Ndemanga aliwataka waendesha pikipiki wanavyoenda kujifunza kuandesha chombo hiko cha moto wanapaswa kuzingatia  somo la alama barabarani kwani hii itasaidia sana kupunguza ajali 

 

Mgeni Rasmi Mhe, Ndemaga aliyasema hayo katika siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa usalama Barabarani Kimkoa katika Wilaya ya Ruangwa iliyofanyika kuanzia 20/11/2017 hadi 24/11/2017.

 

Pia Mhe, Ndemaga alisisitizi suala la kujifunza alama za barabarani lisiwe ni la madereva tu wanaoendesha chombo hiko hata wananchi wanapaswa kujifunza na kuzielewa alama hizo ili kufanikiwa kupunguza ajali za barabarani.

 

“Lindi isiyo na jali za barabarani inawezekana na katika kufanikisha hili ni wajibu wa kila mwananchi wa Mkoa wa Lindi kujifunza umuhimu wa alama hizo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kwa ajali zinazotokea”alisema Ndemanga.

 

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Lindi aliwataka waendesha pikipiki kwa ajili ya kujipatia riziki kuheshimu kazi hiyo na kuiona kama ni kazi nyingine kwani ndiyo sehemu inayowaingizia kipato na kufanya kuendesha maisha yao ya kila siku.

 

“Kazi mnayoifanya mnapaswa kuiheshimu kwa kiasi kikubwa kwani haina tofauti na kazi ya mtu anaenda ofisini kila siku asubuhi, nidhamu katika kazi yako ni chachu ya maendeleo” alisema Mhe, Ndemanga.

 

 

Vilevile Mgeni Rasmi aliwataka maafisa wa zimamoto kupita katika kila ofisi ya serikali kuangalia kama wanamifumo na vifaa vya kuzimia moto na ofisi itakayokosa vifaa hivyo basi mara moja iweke vifaa hivyo.

 

“Siyo tu maofisini hata katika taasisi zote za serikali kama shule na zahanati inapaswa ziwe na vifaa hivyo kwani hizi ni sehemu za mfano hata kwa jamii, wekeni vifaa vya zima moto katika maeneo hayo muhimu”alisema Ndemanga.

 

Pia Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kupunguza Umasikini na Kutunza Mazingira(APEC) Masalu Regu Rwandiko alitoa shukurani na kuiomba serikali kuendelea kuipatia ushirikiano taasisi hiyo inapofika katika Wilaya au Mmkoa kwa ajili ya kutoa huduma za elimu ya Usalama barabarani, elimu ya ujasiliamali na ulinzi shirikishi kwa waendesha pikipiki.

 

Masalu alisema kwa elimu wanayoitoa katika maeneo mbalimbali inasaidia  kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali barabarani na kwa Wilaya ya Ruangwa ajali zimepungua kwa asilimia 76 .

 

Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe, Joseph Mkirikiti aliwataka wakazi wa Ruangwa kutumia fursa zinazojitokeza kama ya kukopeswa pikipiki ambapo mkopeshwaji atapaswa kulipia kiasi cha fedha laki 4 za kitanzania kwa kuanzia alafu atapewa pikipiki hiyo na ataendelea kulipia kidogokidogo huku akiwa amekabidhiwa pikipiki yake

Aidha Mhe, Mkirikiti aliwataka vijana kuacha kukaa katika vijiwe muda wa kazi, fursa hizo zinajitokeza wanapaswa kuzipokea kwa mikono miwili na kuanza kufanya utekelezaji wake.

 

“Ikifika 2018 sitaki kuona vijiwe na nitavivunja mchana kweupe ndani ya Wilaya yangu sitaki watu wazembe na ndiyo maana nilipambana katika kuvunja vijiwe vyote vya (pull table) sasa ikifika huo mwaka nitamaliza vijiwe vyote vilivyobaki”alisema Mhe, Mkirikiti.

 

Mkuu wa Wilaya alitumia fursa hiyo pia kuwakaribisha wananchi wa Mkoa Lindi na walio nje ya Lindi kuhudhuria katika sikukuu ya Maulidi ambayo kitaifa itafanyika katika Wilaya ya Ruangwa mkesha tarehe 30/11/2017 na sikukuu yenyewe itakuwa 1/12/2017.

 

“Karibuni tushereke siku ya kuzaliwa kwa Mtume Mohammad (S.A.W) tumejiandaa kupokea wageni kila mwenye nafasi anakaribishwa kujumuika na wanarungwa katika siku muhimu kama hiyo”alisema Mhe, Mkirikiti.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa