• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MHE. NDEMANGA AWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA RUANGWA KWA UBUNIFU WA VIFUNGASHIO

Posted on: August 6th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga, amewapongeza wajasiriamali wa Wilaya ya Ruangwa kwa kuwa na vifungashio bora vya bidhaa zao katika maonesho ya Nane Nane. Mhe. Ndemanga ameyasema hayo leo, tarehe 6 Agosti 2024, alipotembelea banda la Ruangwa kama mgeni rasmi wa maonesho ya Nanenane kanda ya kusini katika Viwanja vya Ngongo, Lindi.


Amewatia moyo wajasiriamali hao kwa ubunifu wao na kusema kwamba mara nyingi kumekuwa na mfanano wa vifungashio katika mabanda mbalimbali, lakini Ruangwa wamejipambanua kwa utofauti wao na kuwapa pongezi nyingi.


Aidha, Mhe. Ndemanga amewapongeza Mbwemkuru AMCOS kwa kazi nzuri ya kusimamia ushirika huo na kutoa wito kwa vyama vingine vya ushirika kujifunza kutoka kwao. Ametoa pongezi hizo baada ya kupokea maelezo na elimu ya ushirika kutoka kwa Katibu wa Mbwemkuru AMCOS, Ndugu Shabani Rutuba, aliyekuwa katika banda la Ruangwa akitoa elimu kuhusu ushirika, stakabadhi ya ghala, na mfumo wa masoko wa TMX.


Ndugu Rutuba ameeleza kuwa kwa msimu huu wamekusanya jumla ya kilo 1,947,524 za ufuta na kupata mapato ya Tsh 6,687,833,538, na hivyo kuwa AMCOS kinara katika makusanyo ya ufuta kwa Wilaya ya Ruangwa.


Ikumbukwe, maonesho ya Nane Nane yameendelea kuwa jukwaa muhimu kwa wajasiriamali kuonyesha ubunifu na ubora wa bidhaa zao. Ufanisi wa wajasiriamali wa Wilaya ya Ruangwa katika kubuni vifungashio bora ni mfano mzuri wa jinsi maonesho haya yanavyotoa fursa kwa washiriki kuboresha bidhaa zao na kuongeza ushindani katika soko. Mhe. Ndemanga amewahimiza wajasiriamali hao kuendelea kushiriki kikamilifu katika maonesho kama haya, ambayo yanaongeza uelewa na kujenga uwezo wa wajasiriamali kuboresha biashara zao na kuchangia maendeleo ya kiuchumi katika Wilaya na nchi kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa