• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Mhe, Kigwagala Ameagiza Kukarabatiwa Kwa Vyumba Vya Upasuaji Katika Vituo Vya Afya Vya Ruangwa

Posted on: October 6th, 2017

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Hamisi Kigwangala ameuangiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kumalizia chumba cha upasuaji cha Kituo cha Afya Mandawa kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia 06/10/2017.

Pia aliagiza kumaliziwa kwa chumba cha upasuaji cha Kituo cha Afya Mbekenyera kwa muda wa miezi 3 kwa kubadilisha vyumba vilivyokusudiwaa kwa wodi za wazazi kuwa jengo la upasuaji.

Mhe, Naibu Waziri aliyasema haya wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika Wilaya ya Ruangwa tarehe 06/10/2017 alipotembelea vituoa vya Afya vilivyopo katika Wilaya hiyo ambavyo ni Kituo cha Afya cha Luchelegwa, Nkowe, Mbekenyera, na Mandawa pia alipata nafasi ya kutembelea zahanati ya Nandagala.

Naibu Waziri alisema katika utawala huu wa awamu ya tano ni lazima kila kituo cha Afya kiwe na chumba cha upasuaji, hivyo ni bora kuwa na chumba kidogo kuliko kukosekana kabisa chumba cha upasuaji.

“Mhe Mkuu wa Wilaya wewe hapa hauna vituo vya Afya una zahanati zenye majengo mengi vituo hivi vinamapungufu mengi ila ni lazima kuwepo na vyumba vya upasuaji ili kusaidia na kukidhi mahitaji ya wananchi” alisema Kigwangala.

Pia Naibu Waziri Kigwangala alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri kuwezesha kupatikana kwa maji katika vituo vyote vya afya vilivyopo katika wilaya hiyo alisisitiza kupatikana kwa maji katika hospitali kubwa na kubadilisha mabomba yaliyopo sasa katika vituo na hospitali ya wilaya.

Vile vile Naibu Waziri Kigagwala aliutaka uongozi wa hospital kufanya mchakato wa kufunga mfumo wa kielektroniki(GoT HOMIS) kwenye maeneo mengine na si kuishia mapokezi tu kama ilivyo sasa ili kudhibiti vyema mapato yanayoingia katika vituo hivyo na Hospitali ya Wilaya.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya Dr, Japhet Simeo alimuomba Mhe, Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii na Jinsia Dr, Kigagwala awasaidie upatikanaji wa ramani rahisi zenye gharama nafuu kwa wananchi.

Dr, Simeo alisema ramani zilizoletwa Halmashauri zina na makadirio makubwa ya fedha ambayo kwa uhalisia utekelezaji wake unakuwa ni mgumu kwa wananchi.

“Sera ya sasa inawataka wananchi waanze kufanya shughuli za kimaendeleo kama ujenzi wa Zahanati mpaka kwenye boma alafu Halmashauri zimalizie ila kwa makisio ya fedha zinazokuwa zinaletwa inakuwa ngumu kwa wananchi kutekeleza Mhe, Kigagwala naomba suala hili ukatusaidie lipatiwe ufumbuzi kutokana na hali za wananchi wetu”alisema Dr, Simeo

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa