• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MGOGORO WA MIRATHI WASULUHISHWA NANDAGALA KUPITIA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA

Posted on: February 28th, 2025

Mgogoro wa mirathi uliokuwa ukiikumba familia ya Abdallah Chitanda katika kijiji cha Nandagala “B,” Kata ya Nandagala, wilayani Ruangwa, umesuluhishwa kupitia kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia, leo Februari 27, 2025, katika viwanja vya stendi ya Nandagala.


Mgogoro huo ulihusu mgawanyo wa mashamba ya marehemu, ambapo ndugu sita wa familia hiyo walishindwa kufuata utaratibu wa kisheria, hali iliyopelekea mdogo wao wa mwisho kukosa mirathi kabisa, huku kaka yao mkubwa akijitwalia karibu nusu ya eneo lote na kujimilikisha mwenyewe, Kupitia msaada wa kisheria uliotolewa leo pande zote zimekubaliana kutekeleza mgawanyo wa mali kwa mujibu wa sheria, hatua iliyorejesha amani ndani ya familia.


Aidha, Mmoja wa wanafamilia Bi.  Fatuma Abdallah, amepongeza juhudi za Serikali kupitia kampeni ya Mama Samia kwa kuwawezesha kupata haki zao bila gharama za kisheria. 

“Msaada huu umeokoa familia yetu na kuzuia uhasama uliokuwa ukianza kujengeka kutokana na mgogoro wa mirathi”. Amesema Bi. Fatuma


Naye, Mratibu wa kampeni hiyo Wilaya ya Ruangwa Ndugu. Antony Elias amesema msaada wa kisheria unaendelea kutolewa kwa wananchi wenye changamoto mbalimbali, ikiwemo mirathi, ardhi, ndoa, na masuala mengine ya kisheria, huku elimu ikitolewa kwa kila mwananchi, lengo ni kuhakikisha kila mwananchi anapata haki kwa mujibu wa sheria na kuimarisha mshikamano katika jamii.


Hata hivyo, Wananchi wa Nandagala wamehimizwa kutumia fursa hiyo ya msaada wa kisheria ili kuepusha migogoro na kuhakikisha haki inatendeka kwa mujibu wa sheria za nchi.


Kampeni ya Mama Samia Legal Aid inaendelea kutekelezwa wilayani Ruangwa, ikiwa na lengo la kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya kisheria na huduma za msaada wa kisheria kwa urahisi, ili kuimarisha utawala wa sheria na kupunguza migogoro katika jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa