• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Mapato vya ndani huarakisha maendeleo, mmbuni vyanzo vipya

Posted on: June 17th, 2022

Mwalimu Uzima Justine ameshauri serikali za vijiji kubuni vyanzo vya mapato ya kijiji ili viweze kuwasaidia katika kuanzisha na kuendeleza miradi katika maeneo yao.

Alisema "kuwa na vyanzo vya mapato vya kijiji kutasaidia kuchochea maendeleo zaidi katika vijiji vyao kwasababu kutakuwa na miradi wanayotekeleza wenyewe kwa fedha za ndani".

Ameyasema hayo leo 17/06/2022 wakati wa mafunzo ya utawala  bora yanayoratibiwa na Jukwaa la Elimu ya Uraia Tanzania (CETA)  yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya mjini Ruangwa.

Alisema "kupitia vyanzo hivyo vya mapato, watakusanya mapato ya kijiji ambayo wanapaswa kuyatumia vizuri kwa kufuata sheria".

"Hizo si fedha za matumizi yenu binafsi bali ni fedha kwa ajili ya maendeleo ya kijiji, msije kuwa mnagawana posho tu, wananchi wanatakiwa kujua kinachokusanywa na kinavyotumika"

Pia aliwataka kuwa na sheria ndogo na  kuzizingatia sheria hizo kwani zitawaongoza katika kutenda haki kwa wananchi wao.

Naye mshiriki kutoka Namkatila ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Bi. Mwanahamisi Soko aliushukuru uongozi  wa Jukwaa la Elimu ya Uraia Tanzania (CETA) kwa kuwapatia mafunzo hayo na kuwaomba washiriki wengine kupeleka mrejesho kwa wajumbe wengine wa serikali za kijiji ambao hawajapata nafasi ya kushiriki mafunzo hayo.

Alisema Bi. Mwanahamisi, "mafunzo tuliyoyapata ni urithi mkubwa  kwani yatadumu kwasababu si kitu cha kuisha na pia tutatumia elimu hii katika utendaji ili vijiji viwe bora zaidi".

Pia Bi Mwanahamisi  alisema suala la uongozi huwa si la milele, uongozi unabadilika badilika hivyo aliuomba  uongozi wa CETA kutoishia kipindi hiki kwamba wawe wanatoa mafunzo kila uongozi unapobadilika ili vijiji vyote vizidi kuwa bora.

Mafunzo haya yanaratibiwa na Jukwaa la Elimu ya Uraia Tanzania (CETA) yanayohusisha wenyeviti wa vijiji, Watendji wa Vijiji na Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Vijiji na yamelenga kuwafikia viongozi wa serikali za vijiji 90 katika Wilaya ya Ruangwa.

Mpaka sasa washiriki 445 wamepatiwa mafunzo na vijiji 67 vimeshiriki kwa ukamilifu mafunzo hayo.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa