• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAMENEJA NA WAHASIBU 130 WA RUNALI WAHITIMU MAFUNZO YA PAVU

Posted on: October 24th, 2025

Mameneja na wahasibu 130 wa RUNALI kutoka Wilaya za Ruangwa, Nachingwea na Liwale wamehitimu mafunzo ya PAVU yaliyolenga kuongeza ujuzi katika usimamizi na uadilifu wa fedha za vyama vya ushirika (Amcos).


Mafunzo hayo yaliyofanyika kuanzia Oktoba 10 hadi 24, 2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, yalihusisha washiriki 130 wakiwemo wanaume 127 na wanawake 3. Lengo lake kuu lilikuwa kuwajengea uwezo wa kitaaluma wahasibu na mameneja ili kuimarisha uwazi, uadilifu na utunzaji sahihi wa kumbukumbu za kifedha katika Amcos.


Aidha, viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mh. Hassan Ngoma, pamoja na Profesa kutoka Chuo Kikuu cha Ushirika cha Moshi (MoCU) na viongozi wa RUNALI, wamesisitiza umuhimu wa mafunzo hayo katika kuboresha usimamizi wa vyama hivyo.


Vilevile, viongozi hao wamepongeza hatua ya kutoa mafunzo hayo wakieleza kuwa yatasaidia kuzuia hati chafu, kuongeza ufanisi wa kifedha na kuimarisha maendeleo ya wakulima kupitia Amcos.


Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mheshimiwa Hassan Ngoma, amewataka wahasibu na mameneja kutumia maarifa waliyopata kuboresha ufanisi katika vyama vyao vya ushirika.


“Elimu hii mliyoipata isiishie kwenye vyeti pekee, bali iwe chachu ya mabadiliko kwenye usimamizi wa fedha na kumbukumbu za Amcos. Tunataka kuona vyama vyenu vikisimamia kwa uwazi, uadilifu na kwa manufaa ya wakulima,” amesema Mh. Ngoma.


Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo kama RUNALI na MoCU katika kuhakikisha elimu ya fedha na usimamizi bora inawafikia viongozi wote wa vyama vya ushirika nchini.


Kwa ujumla, mafunzo hayo yamechukuliwa kuwa hatua muhimu ya kuleta mageuzi chanya katika sekta ya ushirika, hasa katika kuhakikisha matumizi sahihi na yenye tija ya fedha za wakulima.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • MAMENEJA NA WAHASIBU 130 WA RUNALI WAHITIMU MAFUNZO YA PAVU

    October 24, 2025
  • KILA LA HERI DARASA LA NNE

    October 21, 2025
  • KILA LA HERI DARASA LA NNE

    October 21, 2025
  • ZIMEBAKI SIKU 15 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 14, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa