• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAJALIWA: RAIS SAMIA AMETOA SH. BILIONI MBILI UJENZI WA MIRADI YA MAENDELEO NANGANGA.

Posted on: July 4th, 2022

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata ya Nanganga wilayani Ruangwa.

Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Julai 4, 2022) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa kata hiyo akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika kata hiyo ikiwemo ya afya, elimu na maji.

“Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa umwagiliji Nanganga, tutumie vizuri bonde letu. Vijana changamkieni fursa hii kwa kuanzisha kilimo cha mbogamboga na mazao mengine.”

 Mheshimiwa Majaliwa ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa uendelee na mpango wa ujenzi wa soko la mboga mboga katika Kata ya Nanganga ili kuwawezesha wakulima wa mazao hayo kupata sehemu ya uhakika ya kufanyia biashara.

Amesema Serikali imetoa shilingi milioni 447 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa usambazaji maji Nanganga na shilingi milioni 31 kwa ajili ya kusambaza maji katika kijiji cha Mbecha na shilingi milioni 470 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Mchenganyumba.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka wanafunzi wajitahidi kusoma kwa bidii kwa sababu mbali na Serikali kutoa Elimsingi Bila Ada pia imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya kutolea elimu nchini.

Mheshimiwa Majaliwa amekagua mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Nangumbu, zahanati ya kijiji cha Mtakuja pia, ametembelea shule ya msingi Ndandawale pamoja na kuwasamia wananchi wa kijiji cha Chimbila na kuwasisitiza waendelee kufanya kazi kwa bidii Serikali ipo pamoja nao.

Awali, Diwani wa Kata ya Nanganga, Bw. Kambona aliishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika kata hiyo ikiwemo miradi ya maji ambayo imeweza kutatua changamoto ya uapatikanaji maji.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa