• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA RUANGWA YAFUNGULIWA RASMI

Posted on: August 4th, 2025

Msimamizi wa Uchaguzi Mkuu Jimbo la Ruangwa, Mwl. George Mbesigwe, amefungua rasmi mafunzo kwa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya kata kwa kata zote 22 za Jimbo hilo mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Shule ya Wasichana Ruangwa leo tarehe 04 Agosti 2025.

Mafunzo hayo yamepangwa kufanyika kwa muda wa siku tatu, yakilenga kuwaandaa wasimamizi hao kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya uchaguzi kwa mujibu wa sheria na taratibu. Sambamba na mafunzo hayo, wasimamizi wote wamekula viapo viwili muhimu, kiapo cha kujitoa uanachama au kutokuwa mwanachama wa chama cha siasa na kiapo cha kutunza siri.

Aidha, akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo, Mwl. Mbesigwe amesisitiza kuwa ufanisi wa uchaguzi unategemea kwa kiasi kikubwa uelewa wa kina wa sheria, kanuni, miongozo na taratibu zinazotawala mchakato wa uchaguzi. Ameeleza kuwa kila msimamizi ana wajibu wa kuhakikisha mchakato unakwenda kwa haki na kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Mwl. Mbesigwe, ni wajibu wa kila msimamizi kuhakikisha kuwa kila hatua ya uchaguzi inazingatia misingi ya uwazi, usawa na uaminifu. 

“Wasimamizi wa uchaguzi ni nguzo muhimu katika kulinda amani, demokrasia na haki ya kila Mtanzania kupiga kura, lazima mfanye kazi kwa weledi, uadilifu na uzalendo,” amesema Mwl. Mbesigwe.


Vilevile, amewataka wasimamizi hao kuzingatia kwa makini mafunzo wanayopewa, huku akisisitiza kuwa uelewa mdogo wa taratibu unaweza kuathiri mwenendo mzima wa uchaguzi. Ameongeza kuwa hatua yoyote ya uzembe au ukiukwaji wa taratibu inaweza kusababisha athari kubwa kwa jamii.


Hali kadhalika, Mwl. Mbesigwe amesisitiza kuwa viapo walivyokula si vya kawaida, bali ni ahadi ya kisheria inayowalazimu kuwa waaminifu, kutunza siri na kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu mkubwa. Amewataka kila mmoja kutumia muda wa mafunzo kujifunza, kuuliza na kujadiliana ili kufanikisha uchaguzi wa haki.


Kwa ujumla, mafunzo hayo yanatarajiwa kuwajengea uwezo wasimamizi wa uchaguzi kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu wajibu wao, mazingira ya kazi, na namna ya kushughulikia changamoto mbalimbali wakati wa mchakato wa uchaguzi, huku dhamira kuu ikiwa ni kuhakikisha uchaguzi huru, haki na wa kuaminika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA RUANGWA WALA KIAPO

    August 04, 2025
  • MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA RUANGWA YAFUNGULIWA RASMI

    August 04, 2025
  • RUANGWA YATOA ELIMU YA KILIMO BORA CHA ALIZETI NANE NANE

    August 03, 2025
  • MKURUGENZI CHONYA AKAGUA UJENZI WA HOSTELI ZA NAMUNGO FC, ATOA MAELEKEZO YA KUKAMILISHA KABLA YA AGOSTI KUISHA

    July 31, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa