• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAAFISA WAANDIKISHAJI WAPEWA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU RUANGWA

Posted on: May 14th, 2025

Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa wamepewa mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.


Mafunzo hayo yamefanyika leo, Mei 14, 2025, katika bwalo la Shule ya Sekondari ya Wasichana Ruangwa, yakihusisha pia wakufunzi kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Maafisa TEHAMA, Maafisa Ugavi pamoja na Maafisa Waandikishaji wa ngazi ya Jimbo.


Aidha, lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwawezesha maafisa husika kupata uelewa wa kina kuhusu taratibu sahihi za uandikishaji wapiga kura, sambamba na matumizi ya teknolojia ya kisasa inayotumika katika usajili huo. Washiriki wameelekezwa namna ya kutumia Mfumo wa Usajili wa Wapiga Kura (VRS), ambao umeboreshwa ili kuongeza usahihi wa taarifa na kupunguza changamoto za kiufundi wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Vilevile, mada mbalimbali zimewasilishwa kwa lengo la kuwajengea ujuzi wa vitendo washiriki hao, ikiwa ni pamoja na ujazaji wa fomu za usajili kwa usahihi, utunzaji wa vifaa vya kazi, na mbinu za kushughulikia changamoto zinazoweza kujitokeza kwenye vituo vya uandikishaji. Washiriki pia wamekumbushwa umuhimu wa kushirikiana kwa karibu na viongozi wa maeneo yao ili kuongeza mwitikio wa wananchi kushiriki zoezi hilo.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili kwa Wilaya ya Ruangwa unatarajiwa kuanza rasmi Mei 16 na kukamilika Mei 22, 2025. Katika kipindi hicho, wananchi wenye sifa ya kupiga kura wanahimizwa kujitokeza katika vituo vilivyopangwa ili kujiandikisha, kurekebisha taarifa zao au kuhakiki taarifa zilizopo.


Hata hivyo, Tume imeeleza kuwa dhamira yake ni kuhakikisha kila Mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura anapata fursa ya kuwa katika daftari hilo.

Kwa upande mwingine, Maafisa Waandikishaji walioshiriki mafunzo hayo wametakiwa kuzingatia maadili, weledi na uaminifu katika kutekeleza jukumu hilo muhimu kwa mustakabali wa taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • WILAYA YA RUANGWA KUNUFAIKA NA MRADI WA URASIMISHAJI MAKAZI HOLELA

    June 24, 2025
  • WATUMISHI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KUJIFUNZA

    June 23, 2025
  • DED RUANGWA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU YA RUANGWA VETERAN’S

    June 21, 2025
  • DC NGOMA AZINDUA UWANJA WA MICHEZO WA RUANGWA VETERANS SPORTS CLUB

    June 21, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa