• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAAFISA MIFUGO RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO KUELEKEA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO

Posted on: July 11th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kupitia Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imeendesha mafunzo kwa Maafisa Ugani Mifugo 19 watakaoshiriki katika zoezi la kitaifa la utambuzi na uchanjaji wa mifugo. Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 11 Julai 2025 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo watendaji hao katika matumizi ya mfumo wa kisasa wa uchanjaji na utambuzi wa mifugo.


Akifungua rasmi mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Frank Chonya, amewataka Maafisa Ugani kufanya kazi kwa bidii, weledi na kwa kushirikiana kwa karibu na wafugaji. Amesisitiza kuwa kampeni hiyo ya kitaifa, inayotolewa kwa ruzuku na Serikali ya awamu ya Sita, inalenga kuhakikisha wafugaji wanapata huduma bora ili kuboresha afya ya mifugo na kuinua kipato cha kaya za wafugaji.


Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, kampeni ya chanjo kitaifa imezinduliwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Simiyu, ikiwa ni hatua muhimu ya kitaifa kulinda afya ya mifugo.


Aidha, ng’ombe wanatarajiwa kuchanjwa dhidi ya homa ya mapafu kwa bei ya ruzuku ya shilingi 500 kwa mnyama; mbuzi na kondoo watachanjwa dhidi ya Sotoka kwa shilingi 300 kwa mnyama; huku kuku wakichanjwa dhidi ya kideri, ndui na mafua makali kwa gharama zote kufidiwa na Serikali.


Vilevile, Serikali imetangaza kutoa vitendea kazi kwa wataalamu wa mifugo, vikiwemo vishikwambi na usafiri wa pikipiki, ili kuongeza ufanisi katika usimamizi wa zoezi la uchanjaji na huduma kwa wafugaji.


Mpaka sasa, Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imepokea dozi 110,000 za chanjo ya kuku aina ya Tatu Moja, dozi 3,000 za homa ya mapafu (CBPP) kwa ng’ombe, na dozi 9,500 za Sotoka kwa mbuzi na kondoo. Tayari zoezi la chanjo ya kuku limeanza kutolewa, ambapo hadi sasa wafugaji 2,036 wamefikiwa na jumla ya kuku 35,773 wamechanjwa.


Kwa sasa, maandalizi ya mwisho yanaendelea, yakiwemo ukamilishaji wa mfumo wa utambuzi wa mifugo na usambazaji wa vifaa vya uchanjaji, ili chanjo za homa ya mapafu na Sotoka ziweze kuanza kutolewa mwezi huu wa saba.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • ZIMA MOTO WAENDESHA MAFUNZO YA TAHADHARI YA MAJANGA KWA WATUMISHI RUANGWA

    July 15, 2025
  • MAAFISA MIFUGO RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO KUELEKEA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO

    July 11, 2025
  • MAAFISA MIFUGO RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO KUELEKEA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO

    July 11, 2025
  • PONGEZI

    July 11, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa