• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAAFISA LISHE WATOA ELIMU KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA

Posted on: November 6th, 2025

MAAFISA Lishe kutoka Hospitali ya Wilaya ya Rungwa naKituo cha Afya Ruangwa Mjini, leo Novemba 06, 2025 wametoa elimu ya lishe kwa watumishi wa Halmashauri yaWilaya ya Ruangwa, ikiwa ni sehemu ya kampeniendelevu ya kuhamasisha ulaji bora na afya njema kwawatumishi wa umma.


Elimu hiyo imetolewa katika ukumbi wa Halmashauri yaWilaya ya Ruangwa, ikilenga kuwajengea watumishiuelewa mpana kuhusu umuhimu wa mlo kamili, ulajiunaozingatia makundi yote ya chakula, na namna lishebora inavyoweza kuongeza ufanisi na tija katika utendajiwa kazi za kila siku.


Akizungumza katika kikao hicho, Afisa Lishe kutokaHospitali ya Wilaya ya Rungwa, Bi. Martha Theophil,amesema changamoto kubwa inayowakabili watumishiwengi ni kutopata muda wa kula chakula sahihi kutokanana majukumu mengi ya kazi, jambo linalochangiakuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukiza kama vile shinikizo la damu, kisukari na unene uliopitiliza.

Kwa upande wake, Afisa Lishe kutoka Kituo cha AfyaRuangwa Mjini, Bi. Luciana Joseph amewataka watumishikuzingatia matumizi ya vyakula vya asili vinavyopatikanakatika maeneo yao, hususan mboga mbichi, matunda, nafaka zisizokobolewa na protini za mimea na wanyama, badala ya kutegemea vyakula vya viwandani ambavyohavina virutubishi vya kutosha.


Aidha, Maafisa hao walisisitiza umuhimu wa kufanyamazoezi mara kwa mara, kunywa maji ya kutosha, nakupunguza matumizi ya chumvi, mafuta na sukari kupitakiasi, wakibainisha kuwa tabia hizo ndogo za kiafya zinamchango mkubwa katika kujikinga na magonjwa sugu.

Watumishi wa Halmashauri walioshiriki mafunzo hayowalieleza kufurahishwa na elimu waliyopata, wakisemaimekuwa ni fursa muhimu ya kujitathmini kuhusumwenendo wao wa ulaji na kujipanga upya kuboreshaafya zao kwa manufaa binafsi na ya taasisiwanazozitumikia, huku wakipata fursa pia ya kuulizamaswali mbalimbali.

Mafunzo haya ni sehemu ya jitihada za Halmashauri yaWilaya ya Ruangwa katika kuboresha afya za watumishiwake, ili kuongeza ari, tija na ufanisi kazini kupitiamwamko mpya wa lishe bora na maisha yenye afyanjema.


Mbali na mafunzo, Maafisa hao walitoa huduma yaUpimaji wa Magonjwa yasiyoambukiza kwa watumishiwote waliojitokeza kushiriki, ikiwemo Shinikizo la Damu(Presha) pamoja na Uzito.

Matangazo

  • NAFASI ZA KUJITOLEA HALMSHAURI YA WILAYA YA RUANGWA February 13, 2026
  • FOMU YA USAJILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI February 02, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • ASHALONGO FC VS KIBWANA FARM FC, HAKUNA MBABE

    February 08, 2026
  • RAS LINDI AWAHIMIZA MAAFISA HABARI KUIMARISHA UHUSIANO NA VYOMBO VYA HABARI

    February 05, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa