• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAADHIMISHO YA MWAKA MMOJA WA HUDUMA ZA UPASUAJI KATIKA KITUO CHA AFYA NANDAGALA

Posted on: June 17th, 2024

"Tuna kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwaongoza na kuwasimamia watoa huduma ya upasuaji katika kituo chetu hiki na mpaka kufikia leo hii wagonjwa zaidi ya 70 wamepatiwa huduma hiyo na kutoka wakiwa salama salmini, lakini pia pongezi kubwa kwa yule mteja wetu wa kwanza kabisa ambaye alikuwa na imani kubwa na watoa huduma wa kituo chetu cha Afya na kuwa balozi mzuri kwa wananchi wengine kuwaaminisha ya kwamba Wataalamu wetu wa Afya katika kituo hiki wanatoa huduma ya upasuaji kwa weredi mkubwa"


Hayo yamebainishwa leo Juni 17, 2024 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Andrew Chikongwe ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika Kikao cha maadhimisho ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanza kutolewa huduma ya upasuaji katika Kituo cha Afya Nandagala, kilichofanyika katika kituo hicho.


Kituo hicho kimefunguliwa December 27, 2016 na kuanza kutoa huduma kama Zahanati na ilipofika mwaka 2022, kikaboreshwa zaidi na kuanza kutoa huduma kwa jamii kama Kituo cha Afya.


Mpaka sasa Kituo kina jumla ya Watumishi 14 na zaidi ya wananchi 20,000 wanapata huduma kupitia Kituo hicho, huduma zinazotolewa ni pamoja na huduma ya

kujifungua (kwa njia ya kawaida na upasuaji) ambapo zaidi ya wakinamama 700 wamejifungulia katika kituo hicho, huduma ya kuona wagonjwa wa nje(OPD), huduma ya nasaha na upimaji wa VVU, huduma ya IPD(Wodi ya wakibaba, wakimama na watoto) na huduma nyingine nyingi.


Huduma ya upasuaji kwa mara ya kwanza ilifanywa na Dkt. Paul Christian Mbinga akishirikiana na Wataalam wengine kwa Bi Fikiri Bakari mkazi wa kijiji cha Ng'au mnamo Juni 12, 2023.


Aidha, Mhe. Chikongwe amemuomba Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Feisal Said kuhakikisha Kituo cha Afya Nandagala kinakuwa na daktari bingwa wa kinywa na meno na hii ni kufuatia hatua ya kituo hicho kupokea kiti maalum kwa ajili ya huduma hiyo.


Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Feisal Said ametoa wito kwa Watumishi wa Kituo cha Afya Nandagala kufanya kazi kwa bidii, kupambana na kushirikiana vyema na Wataalam kutoka ngazi ya Wilaya ili kuleta mafanikio makubwa.


"Mkitaka mfanikiwe fanyeni makubwa kazini na siri ya kufanikiwa ni kupambana tu" amesema Dkt. Feisal.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa