Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Victoria Mwanziva (kulia), kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe. Hassan Ngoma, amekabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mhe. Mohamed Moyo, leo tarehe 29 Mei 2025, katika uwanja wa shule ya msingi Chiumbati iliyopo Kijiji cha Chiumbati, Wilaya ya Nachingwea.
Tukio hilo ni sehemu ya mwendelezo wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo inazinduliwa, kuwekwa mawe ya msingi na kukaguliwa ili kuhamasisha uwajibikaji, uzalendo na maendeleo kwa wananchi.
Kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 inasema: “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.”
Ruangwa
Anuani ya Posta: S.L.P 51
Simu ya Mkononi: 0732932312
simu: 0732932312
Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa