• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

KIWENGWA FC YAIBUKA MABINGWA JIMBO CUP 2024 RUANGWA

Posted on: November 25th, 2024





Timu ya Kiwengwa FC kutoka Soko Kuu Ruangwa imetwaa ubingwa wa mashindano ya Jimbo Cup 2024 baada ya kuibuka na ushindi dhidi ya Stand United kutoka Stendi Kuu ya Mabasi, mchezo huo, umeochezwa leo Novemba 25, 2024, katika Uwanja wa Majaliwa Stadium majira ya saa 10 jioni, umemalizika kwa sare ya goli 1-1 kabla ya kuamuliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati, ambapo Kiwengwa FC wamefunga penati 3 dhidi ya 1 ya Stand United.


Mgeni rasmi wa fainali hiyo, Mbunge wa Jimbo la Ruangwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ametoa zawadi ya shilingi milioni 5 kwa Kiwengwa FC kama mshindi wa kwanza wa mashindano hayo, Stand United, walioshika nafasi ya pili, wamepewa shilingi milioni 4 kama zawadi ya kushiriki mashindano hayo kwa mafanikio.


Aidha, timu ya Red Star kutoka kijiji cha Chikundi Kata ya Mandawa imepewa shilingi milioni 3 baada ya kushika nafasi ya tatu, huku Napoli FC kutoka kijiji cha Mbekenyera wakikabidhiwa shilingi milioni 1.5 kwa kushika nafasi ya nne.


Katika hotuba yake, Mhe. Majaliwa amesisitiza kuwa mashindano haya ni sehemu ya juhudi za kuimarisha mshikamano wa kijamii, kuibua vipaji vya michezo, na kuhamasisha maendeleo ya vijana wilayani Ruangwa. Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya michezo ili kutoa fursa kwa vijana zaidi kuonyesha vipaji vyao.


Mashindano ya Jimbo Cup 2024, ambayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka, yameleta hamasa kubwa kwa wananchi wa Ruangwa, huku yakichangia maendeleo ya sekta ya michezo na kujenga mshikamano miongoni mwa jamii za maeneo mbalimbali ya wilaya. Mwaka huu, mashindano hayo yalivutia timu kutoka kata na vijiji mbalimbali, jambo linalodhihirisha ukuaji wa michezo katika ngazi ya wilaya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa