• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

KATIBU TAWALA WILAYA YA RUANGWA AONGOZA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE KIWILAYA

Posted on: March 6th, 2024

Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani kiwilaya kimefanyika Machi 6, 2024 katika viwanja vya shule ya msingi Likunja Kata ya Likunja wilayani Ruangwa ikiwa na kauli mbiu "Wekeza kwa wanawake kuharakisha maendeleo ya Taifa na Ustawi wa jamii" ambapo Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ni Katibu Tawala Wilaya Mhandisi Zuhura Rashidi kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa Mheshimiwa Zuwena Omari

Katibu Tawala Wilaya amepata nafasi ya kukutana na wajasiriamali pamoja na wataalamu wa idara ya  Afya kitengo cha Ukimwi na Saratani ya Shingo ya kizazi na ameshiriki katika upimaji wa afya yake.

Katika hatua nyingine maadhimisho hayo yamehusisha harambee fupi kwa mwanafunzi mlemavu wa shule ya msingi Likunja Aisha Hassan Swalehe (16) anayesoma darasa la 7 na harambee hiyo imeongozwa na Katibu Tawala Wilaya na kwa upendo na huruma ya Wanawake hao wamemchangia mwanafunzi huyo kiasi cha fedha zaidi shilingi milioni moja.

Lakini pia Maadhimisho hayo yameudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo Wawakilishi kutoka NMB na CRDB, Viongozi wa dini mbalimbali, washiriki kutoka mashirika yasiyo ya serikali pamoja na vyombo vya usalama katika kuimarisha ulinzi na usalama katika sherehe hiyo.

Aidha, katika maadhimisho haya yameambatana na mada tofauti tofauti kutoka kwa wadau mbalimbali ikiwemo "umuhimu wa wosia kwa wanawake" imetolewa na Shirika la msaada wa kisheria, "Wekeza kwa Mwanamke" mada hii imetolewa na CRDB, "Teleza kidigitali" mada hii imetolewa na NMB pamoja na " Wanawake kujali Afya zao kwani Afya ni mtaji" mada hii imetolewa na wataalamu kutoka idara ya Afya.

Katika hatua nyingine Diwani wa Kata ya Likunja Mhe. Issa Mussa Ngongonda ametoa shukrani kwa Kamati ya maandalizi ya sherehe ya Wanawake kwa mpangilio mzuri wa sherehe hizo kwani zimefana kweli kweli na kutoa rai kwa Wanawake kujiweka karibu na taasisi za kifedha ili kupata mikopo ambayo itasaidia kuendesha maisha yao na kuhakikisha mikopo hiyo inarejeshwa kwa wakati sahihi ili kujikwamua katika dimbwi la umaskini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa