• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI AKAGUA UJENZI WA MRADI WA VISIMA RUANGWA

Posted on: December 13th, 2024


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Eng. Mwajuma Waziri, ametembelea na kukagua utekelezaji wa mradi wa uchimbaji wa visima vitano vya maji safi na salama unaotekelezwa Wilayani Ruangwa, lengo likiwa ni kuboresha huduma za maji kwa wananchi, mradi huo, unaogharimu Shilingi milioni 325, umefadhiliwa na Serikali ya Tanzania chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo kila Mbunge amepewa visima 5 jimboni kwake lengo likiwa ni kufikisha huduma ya maji katika maeneo ambayo hayakuwa na huduma hiyo kabisa.


Ziara hiyo ya kikazi imefanyika leo, Desemba 13, 2024, ikihusisha wakuu wa Idara, wataalamu kutoka taasisi mbalimbali, na viongozi mbalimbali wa Wilaya. Katika Wilaya ya Ruangwa, vijiji vitano vinavyonufaika na mradi huo ni Mmawa, Namkatila, Mtawilile, Njawale, na Mpara, ambapo jumla ya wakazi 4,195 wanatarajiwa kunufaika na mradi huo.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhandisi Waziri ameeleza kuwa mradi huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama vijijini unafika kila kona ya Tanzania. 


“Kukamilika kwa mradi huu kutasaidia kumaliza changamoto ya maji katika vijiji vingi vya Wilaya ya Ruangwa na hata Wilaya za jirani,” amesema Eng. Waziri.


Aidha, Eng. Waziri ametoa ahadi kwa wananchi wa Kijiji cha Mmawa, kilichopo Kata ya Nandagala, kuwa mradi huo utaanza kutoa huduma rasmi kabla ya Sikukuu ya Krismasi, Desemba 25, 2024.


Hata hivyo, Mradi huo wa kimkakati ni miongoni mwa hatua za Serikali za kuwasaidia Wabunge kutekeleza miradi ya maendeleo katika majimbo yao, kwa manufaa ya wananchi waliowachagua. Eng. Waziri amewasihi wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha miradi kama hiyo inahifadhiwa na kutumika kwa ufanisi.


Nao, Wakazi wa vijiji vilivyonufaika wameshukuru kwa hatua hiyo na kueleza kuwa itabadilisha maisha yao kwa kuwaondolea changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji.


Akizungumza kwa niaba ya wenzake Bwana Rashidi Juma amesema, “tunaishukru sana Serikali yetu inayoongozwa na mama Samia lakini pia Mbunge wetu Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, hakika tunajivunia sana mradi huu, ukianza kutumika watu wote tutakuwa na amani maana shida ya maji itakuwa imeondoka kwenye vijiji vyetu”. amesema Juma



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa