• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Jiungeni na bima ya shirika afya- Waziri Ummy Mwalimu

Posted on: December 20th, 2018

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu amewataka wakulima kujiwekea uhakika na utaratibu wa kupata huduma ya Afya iliyobora.

Amesema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wilaya ya Ruangwa alipofanya mkutano na Viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) katika ukumbi wa Rutesco mjini Ruangwa leo Desemba 20 2018.

Alitoa Rai ya kuwataka viongozi hao  wajiunge na bima ya afya ambayo ni  Shirika Afya  na kuwaunganisha na familia zao inayopatikana kwa elf 76,800

Aliendelea kuwasisitiza kwa kuwatajia Faida na ubora wa bima hiyo ya afya ambayo mtu anapaswa kujiunga kwa elf 76,800 na mtu huyo atapata huduma ya afya sehemu yoyote ndani ya Tanzania.

"Hii inaitwa jipimie Ainaaina tofauti na vifurushi vya simu na ndiyo maan Mwanzo tulikuwa na CHF  kwa elf 15,000, tukaja CHF iliyoboreshwa elf 30,000 na sasa tuna shirika Afya ya elf 76,800 ambayo mtu anatapata huduma kokote Tanzania na kwenye maduka ya dawa yote yaliyoungwanishwa na mfuko wa Bima ya Afya" amesema Waziri.

Mheshimiwa Waziri aliwataka viongozi wa vyama vya msingi kuwa mabalozi wazuri kwa kuwahamasisha wakulima wao kujiunga na bima ya shirika Afya.

" Najua wananchi wetu watasema hiyo bima ni ghali  nyie ndiyo muwe mabalozi wa kuwaelimisha juu ya faida ya bima hiyo kwasababu mmepata bahati ya kupata elimu ya bima hiyo  na ukitegemea wananchi wa huku wanategemea hela za msimu jitahidi kuwaelimisha kipindi hiki wanachopokea hela za korosho ili wajiunganishe  na bima hiyo" amesema Waziri Ummy

Pia waziri wa Afya amesema mtu akijiunga na bima hiyo ndani ya wiki atapata kadi yake na ndani ya siku 21 ataanza matumizi ya kadi hiyo sehemu yoyote atakayoenda iwe hospitali za serikali, hospitali binafsi na maduka ya dawa yaliounganishwa na mfuko wa bima ya Afya (NHIF).

Naye kiongozi wa Chama cha msingi Ali chikawe aliipongeza serikali kwa kuwaletea Bima hiyo na kuahidi kuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao kwani Bima hiyo inarahisisha sana upatikanaji wa huduma za afya hata zile zenye gharama kubwa.

Aidha aliomba serikali kutowaachia jambo hili wao tu la kuhamasisha wananchi aliomba wananchi wapewe elimu ya bima ya shirika Afya ili kwao iwe rahisi kuendelea kuhamasisha na kutilia msisitizo.

Shirika Afya ni bima ambayo mwananchi anajiunga kwa elf 76,800 kwa mtu mmoja ambaye ni mtu mzima na kwa mtoto elf 50,400 bima hii inamuwezesha mwananchi kupata huduma ya afya ndani ya Tanzania hospitali za serikali, hospitali binafsi na maduka ya dawa yote yaliyoungwanishwa na mfuko wa Bima ya Afya( NHIF).

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa