• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

HALMASHAURI YA RUANGWA YATOA MAFUNZO KWA WATUMISHI WAPYA

Posted on: February 12th, 2025



Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imeendesha mafunzo kwa watumishi wa ajira mpya 164 wa sekta mbalimbali, wakiwemo afya, utawala, kilimo na mifugo, na usafirishaji, ili kuwawezesha kuelewa taratibu za utumishi wa umma.


Mafunzo hayo yamefanyika Februari 12, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri kwa lengo la kuwaelimisha watumishi hao kuhusu kanuni, haki, na wajibu wao katika utumishi wa umma, sambamba na hilo, wamepewa elimu ya hifadhi ya jamii kupitia Mfuko wa PSSSF pamoja na usimamizi wa fedha kutoka kwa wawakilishi wa benki za CRDB na NMB.


Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Frank Edger Komba ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu, amesema Serikali inatarajia watumishi hao kuzingatia weledi, maadili na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao.

“Hii ni fursa muhimu kwenu kuelewa mazingira ya kazi na namna ya kutekeleza majukumu kwa kuzingatia taratibu za utumishi wa umma,” amesema Ndugu Komba.


Kwa upande wake, Mwakilishi wa PSSSF Ndugu John Sombe ameongeza kuwa mfuko huo unahakikisha maslahi ya mtumishi wa umma yanazingatiwa hata baada ya kustaafu.

 “Mnapaswa kufahamu haki zenu za mafao na michango yenu ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza baada ya utumishi wenu,” amesema Ndugu Sombe.


Kwa upande wake, Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Denis Henry Temu, ambaye ni mtumishi mpya wa sekta ya afya, amesema mafunzo hayo yamempa mwanga kuhusu wajibu wake na namna ya kufuata taratibu sahihi.

 “Nilikuwa sijui mambo mengi kuhusu taratibu za utumishi wa umma, lakini sasa nina uelewa mzuri wa haki na wajibu wangu,” amesema Temu.


Ikumbukwe, kupitia mafunzo haya Serikali inahakikisha kila mtumishi anakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu taratibu na kanuni za utumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa