• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Dr Kalemani Azindua Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mkoa wa Lindi

Posted on: August 20th, 2017




Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dr. Medadi Kalemani amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Lindi kutenga fedha zitakazofanya shughuli ya ‘wiring’ katika taasisi za umma katika msimu wa REA III.

Aliyasema hayo katika kijiji cha Chinongwe kilichopo katika Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi alipokuwa anazindua mpango wa REA III.

Dr Kalemani aliwataka wakazi wa Kijiji cha Chinongwe waitumie fursa hiyo vizuri kwa kuweka umeme majumbani mwao, kwani wamepata bahati katika Wilaya zote zilizopo katika Mkoa wa Lindi wao wamepata nafasi ya kwanza ya kupata huduma hiyo.

“Umeme ni uchumi, umeme ni kila jambo tunakila sababu ya kuipongeza Serikali kwa kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata huduma nzuri za jamiii, hivyo msiishie kuweka umeme majumbani tu utumieni kufanya shughuli za kiuchumi”alisema Dr Kalemani.

Vilevile alimtaka Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Mkoa wa Lindi kufanya utaratibu wa kuanzisha madawati ya kuhudumia wateja wenye shida ya kuunganishiwa umeme katika vijiji ambavyo mradi unapita.

“Sitaki kusikia mwananchi anatembea kilometa 30 kwenda mjini kufuatilia suala la kuunganishiwa umeme nataka TANESCO ndiyo muwafuate wateja kwani mteja ni mfalme, mwiko mteja kumfuata TANESCO” alisema Dr Kalemani.

Pia alimtaka mkandarasi atakayekuwa anafanya ‘wiring’ katika makazi ya watu aidhinishwe na TANESCO wenyewe ili kuepuka vishoka na kuepuka suala la bei kutofautiana wakati zoezi hilo likiendelea.

“TANESCO chondechonde msiwawekee wananchi wetu bei kubwa ya kufanya ‘wiring’, bei iwe nafuu ili kila mwananchi aweze kupata huduma hiyo, tunataka kila mwananchi autumie umeme kuanzisha viwanda vidogovidogo”alisema Mh, Kalemani.

Naye Mkurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Disima Namhanga alitoa pongezi kwa serikali kwa kuweza kusimamia na kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma nzuri za kijamii.

“Serikali ya awamu ya tano inataka kila kijiji na vitongoji vyake umeme uweze kuwafikia wakazi wake na ndiyo maana umeme ni uchumi na umeme ni kila kitu wananchi watumie fursa hii vizuri”, alisema Namhanga.

Namhanga alisema vijiji 348 vilivyopo katika Mkoa wa Lindi vinatakiwa vipatiwe umeme, ila Wakandarasi wataanza na vijiji 175 ambavyo kazi yake itafanyika kwa wiki 24, wakimaliza hiyo wataendelea na vijiji 173 vitakavyobaki.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa