• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

DOZI YA PILI YA CHANJO YA POLIO KWA WATOTO WA MIEZI 9 KUANZA MEI 2025 – DC NGOMA ATOA WITO KWA JAMII

Posted on: April 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, ameongoza kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) kilichofanyika leo Aprili 16, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, kwa lengo la kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ongezeko la dozi ya pili ya chanjo ya polio (IPV).


Kikao hicho kimehudhuriwa na wajumbe kutoka Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, viongozi wa dini, Kamati ya Usimamizi wa Huduma za Afya Wilaya (CHMT), wawakilishi wa jamii, pamoja na Timu ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT). Wajumbe hao wamepatiwa elimu kuhusu utekelezaji wa utoaji wa chanjo, ili kuhakikisha kuwa jamii inafikiwa na ujumbe huo muhimu.


Aidha, utoaji wa dozi ya pili ya chanjo ya sindano ya polio (IPV) utafanyika kuanzia Mei 2025 kwa watoto wa umri wa miezi 9. Dozi ya kwanza ya chanjo hiyo hutolewa katika wiki ya 14, hivyo ongezeko hili linaongeza ufanisi wa kinga dhidi ya ugonjwa wa kupooza (poliomyelitis).


Vilevile, chanjo hiyo itaendelea kutolewa kupitia utaratibu wa kawaida wa utoaji wa chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na huduma za Mkoba, na imethibitishwa kuwa salama na Shirika la Afya Duniani (WHO) pamoja na kuidhinishwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) chini ya Wizara ya Afya.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, amesema kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha afya za watoto.


 “Ongezeko hili la dozi ya pili ya chanjo ya polio ni hatua muhimu ya kulinda afya za watoto wetu dhidi ya ugonjwa hatari wa kupooza, Serikali ya Wilaya itaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha kila mtoto anayestahili anapata chanjo hii muhimu,” amesema Mhe. Ngoma.


Mbali na hayo, Serikali ya Wilaya ya Ruangwa imeendelea kusisitiza ushirikiano wa karibu kati ya jamii na wataalamu wa afya katika kuhakikisha watoto wote wanaostahili wanapatiwa chanjo hiyo, ili kujenga jamii yenye afya bora na kuendeleza mapambano dhidi ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa