• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

DC NGOMA AZINDUA UWANJA WA MICHEZO WA RUANGWA VETERANS SPORTS CLUB

Posted on: June 21st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe. Hassan Ngoma ameongoza hafla ya uzinduzi wa uwanja wa michezo wa Ruangwa Veterans Sports Club uliopo Kilimahewa wilayani Ruangwa uwanja huo una ukubwa wa ekari 2.79 na uzinduzi wake umefanyika leo Juni 21 2025 kwa lengo la kuendeleza michezo na kukuza vipaji kwa vijana.


Ujenzi wa uwanja huo umegharimu jumla ya shilingi milioni 6.57 ambapo kati ya hizo milioni 5 zimetokana na michango ya wanachama wa klabu hiyo na zaidi ya milioni 1.5 zimepatikana kupitia nguvu kazi ya kujitolea. Miongoni mwa shughuli zilizotekelezwa ni pamoja na kusafisha eneo, kutengeneza ‘pitch’, kupanda nyasi, kuweka magoli na kuvuta maji kwa matumizi ya uwanja.

Aidha, akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Ngoma amepongeza jitihada za wanachama wa timu hiyo kwa uzalendo, mshikamano na kujitoa kwa vitendo akibainisha kuwa jamii ya Ruangwa inahitaji taasisi kama hizi zinazochangia maendeleo kupitia michezo. Amesisitiza kuwa uwanja huo ni rasilimali ya pamoja inayopaswa kutunzwa na kuendelezwa kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho. “Uwanja huu si kwa ajili ya Veterans pekee bali ni kwa jamii nzima Tutashirikiana nanyi kuhakikisha unaboreshwa zaidi,” amesema Mhe. Ngoma.

Kwa upande mwingine, Katibu Mkuu wa klabu hiyo Ndugu Ramadhan Matola ameeleza kuwa Ruangwa Veterans Sports Club ilianzishwa mwaka 2020 ikiwa na wanachama 18 na hadi sasa ina wanachama hai 42 wakiwemo wanaume 39 na wanawake 3. Amefafanua kuwa maendeleo yaliyopatikana ni matokeo ya mshikamano wa wanachama na usaidizi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa.


Hata hivyo, pamoja na hatua zilizofikiwa changamoto ya ukosefu wa uzio imeelezwa kuwa kikwazo kikubwa kwani uwanja umekuwa ukiingiliwa na mifugo hali inayosababisha uharibifu wa miundombinu. Sambamba na hilo, upungufu wa vifaa vya michezo na ukosefu wa udhamini umeendelea kudhoofisha kasi ya maendeleo ya klabu hiyo.


Kwa ujumla, viongozi wa timu wametoa wito kwa Serikali, wadau wa michezo na wafadhili binafsi kuunga mkono juhudi za wanachama kwa kusaidia ujenzi wa uzio utoaji wa vifaa na uwezeshaji wa programu za kukuza vipaji wilayani Ruangwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • WILAYA YA RUANGWA KUNUFAIKA NA MRADI WA URASIMISHAJI MAKAZI HOLELA

    June 24, 2025
  • WATUMISHI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KUJIFUNZA

    June 23, 2025
  • DED RUANGWA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU YA RUANGWA VETERAN’S

    June 21, 2025
  • DC NGOMA AZINDUA UWANJA WA MICHEZO WA RUANGWA VETERANS SPORTS CLUB

    June 21, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa