• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

DC NGOMA AHITIMISHA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

Posted on: November 22nd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, leo Novemba 22, amefunga rasmi mafunzo ya Jeshi la Akiba katika kijiji cha Namkatila, Kata ya Matambarale, mafunzo hayo, ambayo yamehitimishwa kwa sherehe maalum, yamewezesha askari zaidi ya 100 kuhitimu kwa mafanikio makubwa, yakiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama wa wananchi na maendeleo ya Wilaya ya Ruangwa.


Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mhe. Ngoma amesema kijiji cha Namkatila kimefanya kazi ya kipekee katika maandalizi na utekelezaji wa programu hiyo, amesisitiza kuwa mafanikio hayo yanaimarisha msingi wa maendeleo endelevu kwa Wilaya ya Ruangwa, huku akielezea kufurahishwa na kiwango cha nidhamu na ukakamavu ulioonyeshwa na wahitimu.


 “Mmefunika, haijawahi kutokea,” amesema, akiwapongeza wakufunzi na wananchi kwa kushirikiana kikamilifu kufanikisha mpango huo.


Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea washiriki ujuzi muhimu wa kijeshi kama ujanja wa porini, matumizi ya silaha, usomaji wa ramani, na huduma ya kwanza. Vilevile, wahitimu walijifunza ujasiriamali, jambo ambalo Mhe. Ngoma amesema linachangia kuongeza ustawi wa kiuchumi kwa jamii, sambamba na kudumisha usalama wa eneo hilo.


“Mkawe watiifu na wazalendo kwa nchi yenu. Mafunzo haya ni nyenzo muhimu kwa maendeleo ya Taifa. Hakikisheni mnatii sheria, kanuni, na taratibu, na msitumie mafunzo haya vibaya kwa wananchi,” amesema, akiwahimiza wahitimu kutumia stadi walizopata kuleta manufaa kwa jamii yao.


Aidha, amewataka wananchi wa Ruangwa kushirikiana na vijana hawa waliopitia mafunzo ya Jeshi la Akiba kwa lengo la kuimarisha mshikamano na usalama. Mhe. Ngoma amesisitiza kuwa ukakamavu walionyesha wahitimu unapaswa kuwa chachu ya maendeleo na ustawi wa Wilaya nzima.


Ikumbukwe, Sherehe hizo zimeonesha mshikamano mkubwa wa jamii na mafanikio makubwa ya mafunzo hayo, ambayo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuimarisha amani na usalama kama nyenzo ya maendeleo. Wahitimu wamesifiwa kwa ustahimilivu na juhudi zao, huku wakihimizwa kutumia ujuzi wao kwa njia chanya na yenye tija kwa Taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa